MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Thursday 28 February 2019

Kila mtanzania kutibiwa kwa BIMA ya Afya 2019



Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imejipanga kutekeleza agizo la Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuhakikisha kila mtanzania anapata Bima ya afya. Bima hiyo ambayo itapatikana kwa bei nafuu itamuwezesha kila mtanzania kupata matibabu kwa kutumia kitambulisho chake badala ya sasa ambapo watanzania Wengi wanapata huduma ya afya kwa malipo ya fedha taslimu.

Akizungumza jana wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani Mtwara. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Dkt. Faustin Ndugulile amesema wizara imejipanga kuhakikisha changamoto hiyo inaisha mwaka 2019 na kwamba kila mtanzania atafikiwa.

Mheshimiwa Ngugulile ambaye kitaaluma ni Daktari wa amekili kuwepo malalamiko ya wananchi kuhusu kumudu gharama za huduma za afya na kusisitiza kwamba suluhisho ni kuwa na Bima ya afya

“Tumeboresha huduma hivyo kuna huduma zingine za kibingwa ambazo gharama yake ni kubwa. ndiyo maana tunapambana kuhakikisha kila mtanzania anakwua na Bima ya afya. Amesema Mhe. Ndugulile”

Amesisitiza watumishi wa afya kuhakikisha wanawahudumia wananchi katika maadili ya kazi yao na kusogeza Huduma karibu na wananchi.

“Mfano mzuri ni Bwana Said Akili ambaye ametoka Nanyamba kuja kupata kadi yake hapa Mtwara. Bima inabidi wajipange kuwafuata wananchi huko huko kwenye maeneo yao kama ambavyo wamekuwa wakiwafuata kwenda kuwahamaisha. Kama mmewafuata kuwahamasisha kwa nini msiwafuatae kuwapa kadi zao? wafuateni muwape kwenye mikutano ya hadhara ili kuhamasisha wengine”.

Naye Saidi Akili ambaye alikabidhiwa kadi yake ya Ushirika afya    ameshukuru serikali kwa kuweka utaratibu huo na kuwataka wananchi wengine kuchangamkia fursa.

“wakulima wengi wa korosho tunalima kwa kutumia jembe la mkono na panga. mapato yetu ni kidogo na yanapatikana kwa kipindi maalumu. Bahati mbaya homa haichagui siku hivyo ni vema kuwa na kadi kama hii ili uwe tayari muda wowote”. Amesema said.

Tangu serikali ya awamu ya Tano IIngie madarakani imekuwa ikifanya maboesho mengi katika huduma za Afya ikiwempo kuongeza bajeti katika hudma hiyo, kujenga miundombinu ya afya pamoja na kusambaza vifaa tiba na watumishi sehemu mbalimbali nchini.

No comments:

Post a Comment