Serikali ya Mkoa wa Mtwara imeanzisha operation maalumu ya kuwakamata wafanyabiashara wanaouza sukari kinyume na maelekezo ya serikali. Zoezi hilo lililoanza jana limeweza kuwakamata wafanyabiashara wanane ambao walikutwa wanauza sukari kwa bei ya hadi shilingi 3600 kwa kilo moja.
Akizungumza mara baada ya kumuapisha Mhe. Dunstan Kyobya aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Byakanwa amesema operation hiyo ni endelevu kwa mkoa mzima. Amewataka wananchi watowe taarifa kwa jeshi la polisi juu ya wafanyabishara wanaokiuka maagizo.
maelezo zaidi fungua hiyo video au tembelea youtube channel ya Mtwara RS. Usisahau kusubscribe huko.
Mtwara
MTWARA KUCHELE
Friday, 8 May 2020
Friday, 17 April 2020
Wachina wajitosa kusapoti mapambano dhidi ya CORONA Mtwara
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa
Gelasius Byakanwa ametoa wito kwa Taasisi, Mashirika na watu binafsi
wenye uwezo wa kutengeneza barakoa (Mask) watengeneze kwa wingi. Wito
huo ameutoa leo Aprili 17, 2020 wakati akipokea msaada wa vifaa vya
kujikinga na maradhi ya COVID-19 kutoka kwa kampuni ya Beijing
Construction and Engineering Group CO. LTD inayoshughulika na upanuzi wa
uwanja wa Ndege wa Mtwara.
Amesema mahitaji ya vifaa hivyo kwa sasa
ni makubwa hasa kwa watoa huduma na watu wote ambao kila siku wanafanya
kazi ya kukutana na watu. Aidha, amesisisitiza jamii kuendelea
kujikinga na ugonjwa huo kwa kuzingatia tahadhari zote ikiwemo kuvaa
barakoa huku akiwasisitiza wageni wanaotembelea ofisini kwake
kuhakikisha wanavaa barakoa.
“..na mimi kama Mkuu wa Mkoa,
tutakapoanza wiki inayofuata, hakuna mtu atakayefika kwenye ofisi yangu
bila kuvaa Mask. kuanzia jumatatu tarehe 20, kila mtu atakayefika kwenye
ofisi ya Mkuu wa Mkoa atapaswa kuwa amevaa Mask.” Amesema Byakanwa.
Naye Meneja wa kampuni ya Beijing
Construction Cui Rui Tao ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa hatua
inazochukua dhidi ya ugonjwa wa COVID-19. Amesema wameona umuhimu wa
kusaidia jitihada hizo kwa kutoa msaada wa Barakoa elfu moja, galoni 10
za lita tanotano Pamoja na vitakasa mikono.
Kutazama video ya makabidhiano. Bonyeza hapo. https://www.youtube.com/watch?v=CQXKWDd3r7E
Tuesday, 7 April 2020
Kondakta watakiwa kuzingatia afya ili kujikinga na Korona
Mkuu wa mkoa wa Mtwara amewataka madereva, kondakta na wakatisha tiketi wa magari ya abiria yanayoingia na kutoka Mkoani Mtwara kuzingatia misingi ya afya ili kujilinda wenyewe pamoja na abiria, dhidi ya ugonjwa wa COVID-19.
“Kilichonisikitisha sana, wamiliki
wa magari hamjaongea na wafanyakazi wenu. Sikutegemea niwe stendi, nishuhudie konda
au mkatisha tiketi anagombea abiria, anamshika mkono…. Huyo abiria mkaribishe tu
hakuna kushikana wala kubebeana mizigo.” Amesema Byakanwa.
Sylivia Mamkwe. Mganga Mkuu wa Mkoa akizungumza na waandishi wa Habari
Mkurugenzi Manispaa Mtwara Mikindani Kanali Emmanuel Mwaigobeko akinawa mikono kabla ya kuingia ,ndani ya eneo la kituo cha mabasi Chipuputa
“Upuliziaji huu utakuwa
ukifanyika kila siku asubuhi kwa standi zetu zote za Manispaa ikiwamo standi ya
zamani, Standi kuu ya Chipuputa, na standi ya daladala iliyoko Mikindani”.
Amesema Mwaigobeko.
Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya
Usalama Barabarani Mkoa wa Mtwara, Nassoro Mansoor Hassan ameishukuru serikali
kwa kusimamia zoezi hilo na kusema limegharamiwa na wamiliki wa mabadi kwa kusimamiwa na serikali. Aidha wataendelea kuchukua hatua zaidi kadiri watakavyokuwa
wakipokea maagizo kutoka serikalini.
“Lengo letu ni kuhakikisha
sisi na abiria wetu tunakuwa salama hivyo tutachukua hatua kadiri serikali
itakavyotuongoza” Amesema Nassoro
Monday, 6 April 2020
Sirro awahakikishia ulinzi wakazi Mtwara
Mkuu wa Jeshi la polisi nchini (IGP) Simon Sirro
amewahakikishia ulinzi na usalama wananchi wa mkoa wa Mtwara na kuwataka wafanye
kazi zao bila hofu yoyote. Ameyasema hayo leo Aprili 6, 2020 wakati wa ziara ya
viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini yenye lengo la kuangalia
namna walivyojipanga kukabiliana na uhalifu ndani ya nchi na mipakani.
amewahakikishia ulinzi na usalama wananchi wa mkoa wa Mtwara na kuwataka wafanye
kazi zao bila hofu yoyote. Ameyasema hayo leo Aprili 6, 2020 wakati wa ziara ya
viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini yenye lengo la kuangalia
namna walivyojipanga kukabiliana na uhalifu ndani ya nchi na mipakani.
“kitendo cha kuona wanakuja wanachinja watu
wetu lazima ifike mahali tuseme mwisho na iwe mwisho. Wao wametangaza ligi. Wametangaza
mapambano lazima na sisi tuwe tayari kwa mapambano”. Amesema Sirro.
wetu lazima ifike mahali tuseme mwisho na iwe mwisho. Wao wametangaza ligi. Wametangaza
mapambano lazima na sisi tuwe tayari kwa mapambano”. Amesema Sirro.
Bonyeza hapo chini usikilize
Monday, 30 March 2020
Polisi waimarisha ulinzi mpka wa Tanzania-Msumbiji
Jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya
ulinzi na usalama Vimeimarisha ulinzi katika mipaka ya Tanzania ili kuhakikisha
wahalifu wanaofanya mauaji na vurugu nchini Msumbiji hawapati nafasi ya kuingia
Tanzania.
ulinzi na usalama Vimeimarisha ulinzi katika mipaka ya Tanzania ili kuhakikisha
wahalifu wanaofanya mauaji na vurugu nchini Msumbiji hawapati nafasi ya kuingia
Tanzania.
Hayo yamesemwa leo na Kamishna wa Operesheni na
Mafunzo wa Jeshi la Polisi Liberatus Sabas wakati akikagua kikosi maalumu cha
kupambana na uhalifu nchini kilichowasili mkoani Mtwara kwa ajili ya kuimarisha
ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji.
Mafunzo wa Jeshi la Polisi Liberatus Sabas wakati akikagua kikosi maalumu cha
kupambana na uhalifu nchini kilichowasili mkoani Mtwara kwa ajili ya kuimarisha
ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji.
Amesema wahalifu hao wamekuwa wakivamia kambi za jeshi, vituo vya polisi, kuchoma
moto na kuchukua silaha nchini Msumbiji na pia wameripotiwa kuvamia benki na
kupora fedha huko huko Msumbiji.
moto na kuchukua silaha nchini Msumbiji na pia wameripotiwa kuvamia benki na
kupora fedha huko huko Msumbiji.
“Kule hali si shwali kama ambavyo mmekuwa mkisikia
kwenye vyombo mbalimbali vya habari. Sisi kwa kutambua hilo, na kutambua
umuhimu wa sisi kama Taifa, na umuhimu wa wananchi wa Tanzania kuwa shwali
tumejipanga kuhakikisha tatizo hili haliji huku kwetu.”
kwenye vyombo mbalimbali vya habari. Sisi kwa kutambua hilo, na kutambua
umuhimu wa sisi kama Taifa, na umuhimu wa wananchi wa Tanzania kuwa shwali
tumejipanga kuhakikisha tatizo hili haliji huku kwetu.”
Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwasilisha
taarifa za mtu yeyote ambaye wanamtilia shaka.
taarifa za mtu yeyote ambaye wanamtilia shaka.
Subscribe to:
Posts (Atom)