Mkuu wa mkoa wa Mtwara amewataka madereva, kondakta na wakatisha tiketi wa magari ya abiria yanayoingia na kutoka Mkoani Mtwara kuzingatia misingi ya afya ili kujilinda wenyewe pamoja na abiria, dhidi ya ugonjwa wa COVID-19.
“Kilichonisikitisha sana, wamiliki
wa magari hamjaongea na wafanyakazi wenu. Sikutegemea niwe stendi, nishuhudie konda
au mkatisha tiketi anagombea abiria, anamshika mkono…. Huyo abiria mkaribishe tu
hakuna kushikana wala kubebeana mizigo.” Amesema Byakanwa.
Sylivia Mamkwe. Mganga Mkuu wa Mkoa akizungumza na waandishi wa Habari
Mkurugenzi Manispaa Mtwara Mikindani Kanali Emmanuel Mwaigobeko akinawa mikono kabla ya kuingia ,ndani ya eneo la kituo cha mabasi Chipuputa
“Upuliziaji huu utakuwa
ukifanyika kila siku asubuhi kwa standi zetu zote za Manispaa ikiwamo standi ya
zamani, Standi kuu ya Chipuputa, na standi ya daladala iliyoko Mikindani”.
Amesema Mwaigobeko.
Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya
Usalama Barabarani Mkoa wa Mtwara, Nassoro Mansoor Hassan ameishukuru serikali
kwa kusimamia zoezi hilo na kusema limegharamiwa na wamiliki wa mabadi kwa kusimamiwa na serikali. Aidha wataendelea kuchukua hatua zaidi kadiri watakavyokuwa
wakipokea maagizo kutoka serikalini.
“Lengo letu ni kuhakikisha
sisi na abiria wetu tunakuwa salama hivyo tutachukua hatua kadiri serikali
itakavyotuongoza” Amesema Nassoro
No comments:
Post a Comment