MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Tuesday 7 April 2020

Kondakta watakiwa kuzingatia afya ili kujikinga na Korona



Mkuu wa mkoa wa Mtwara amewataka madereva, kondakta na wakatisha tiketi wa magari ya abiria yanayoingia na kutoka Mkoani Mtwara kuzingatia misingi ya afya ili kujilinda  wenyewe pamoja na abiria, dhidi ya ugonjwa wa COVID-19.

Agizo hilo amelitoa leo Aprili 7, 2020 wakati akizindua mpango wa upuliziaji dawa magari ya abiria kwa mkoa wa Mtwara zoezi ambalo litafanyika kwa kipindi cha mwezi mmoja. Katika uzinduzi huo uliofanyika kituo cha mabasi cha Chipuputa Manispaa ya Mtwara Mikindani amesisitiza wapiga debe wasiwavute abiria na mizigo yao kwani ni kero na hatari kwa kipindi hiki cha maambukizi ya CORONA.
 
“Kilichonisikitisha sana, wamiliki wa magari hamjaongea na wafanyakazi wenu. Sikutegemea niwe stendi, nishuhudie konda au mkatisha tiketi anagombea abiria, anamshika mkono…. Huyo abiria mkaribishe tu hakuna kushikana wala kubebeana mizigo.” Amesema Byakanwa.  

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Sylivia Mamkwe amesema zoezi hilo litafanyika kwa standi zote za wilaya za mkoa wa Mtwara kwa kipindi cha mwezi mzima huku Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Kanali Emmanuel Mwaigobeko akisema wamejipanga kuhakikisha standi kuu za magari na daladala zote za ndani ya manispaa zinatekeleza zoezi hilo.
Sylivia Mamkwe. Mganga Mkuu wa Mkoa akizungumza na waandishi wa Habari
Mkurugenzi Manispaa Mtwara Mikindani Kanali Emmanuel Mwaigobeko akinawa mikono kabla ya kuingia ,ndani ya eneo la kituo cha mabasi Chipuputa

“Upuliziaji huu utakuwa ukifanyika kila siku asubuhi kwa standi zetu zote za Manispaa ikiwamo standi ya zamani, Standi kuu ya Chipuputa, na standi ya daladala iliyoko Mikindani”. Amesema Mwaigobeko.

Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Mtwara, Nassoro Mansoor Hassan ameishukuru serikali kwa kusimamia zoezi hilo na kusema limegharamiwa na wamiliki wa mabadi kwa kusimamiwa na serikali. Aidha wataendelea kuchukua hatua zaidi kadiri watakavyokuwa wakipokea maagizo kutoka serikalini.
Nassoro Mansoor Hassan. Mwenyekiti Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Mtwara 

“Lengo letu ni kuhakikisha sisi na abiria wetu tunakuwa salama hivyo tutachukua hatua kadiri serikali itakavyotuongoza” Amesema Nassoro

No comments:

Post a Comment