MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Sunday 29 January 2017

Madini ya ‘Graphite’ yagundulika Mtwara. ni katika vijiji vya Chiwata na Chidya wilayani Masasi


Viongozi wa kampuni ya Nachi Resource LTD iliyogundua rasilimali kubwa ya madini ya Graphite wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Mtwara mara baada ya kikao.  Waliokaa kutoka kulia ni Godwin Nyero, Msimamizi Mkuu wa kampuni Nachi Resource LTD hapa Nchini. Wa pili kutoka kushoto ni Mbunge wa jimbo la Ndanda, Mheshimiwa Mwambe akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mhe. Seleman Mzee.




Neema ya ugunduzi wa malighafi asilia imeendelea kuonekana mkoani Mtwara baada ya kampuni ya Nachi Resource LTD iliyosajiliwa nchini Tanzania kugundua kiasi kikubwa cha madini ya Kinywe (graphite) katika vijiji vya Chiwata na Chidya vilivyoko Mkoani Mtwara na Vijiji vya Namangale na Utimbula vilivyoko wilayani Lindi mkoani Lindi.

 Godwini Nyero. Msimamizi wa kampuni ya Nachi nchini Tanzania.



Akizungumza katika kongamano ya kutambulisha mradi huu kwa wadau lililofanyika Mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Kagwa mjini Lindi Msimamizi wa Nachi Resouce LTD nchini Tanzania Godwin Nyero amesema Utafiti ulioanza mwaka 2015 umeonesha kuwapo kwa miamba ya mashapo kiasi cha tani milioni 416 yenye ubora wa asilimia 4.9. 

Aidha katika hatua ya kuelekea uchimbaji wanakusudia kuanza tathmini ya mali na fidia mwezi Feb, 2017 wakati tathimini ya athari za mazingira waliyokwisha ianza ikitarajiwa kukamilika Juni, 2017.

Nyero amesema lengo lao ni kuanza shughuli haraka ili kuliwahi soko kabla Msumbiji ambao pia wamegundua rasilimali kubwa ya madini haya.

Aidha, baada ua ufunguzi wa mradi huu unaotarajiwa kutoa ajira za moja kwa moja 270, kampuni ya Nachi Resource ambayo inamilikiwa kwa asilimia mia na Volt Resouce LTD iliyosajiliwa katika soko la hisa la Australia itakuwa ikisafirisha malighafi hiyo kiasi cha tani 100,000 hadi 180,000 kupitia bandari ya Mtwara.


Kwa upande wake Mhandisi wa mazingira kutoka kampuni ya Tanisheq LTD inaayotathimini athari za kijamii na kimazingira, Gwakisa Mwakyusa amesema mradi huu unatarajiwa kutoa ajira za moja kwa moja 270 na faida zingine lukuki zitakazotokana na fursa zitakazochangamkiwa na wananchi wa maeneo haya. Vilevile mradi huu utavutia uwekezaji mwingine wa huduma na uzalishaji mali ambao utapelekea uzalishwaji wa fursa za ajira zaidi kwa wakazi wa maeneo yanayozunguka mradi.

 Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Seleman Mzee.




Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Masasi Mheshimiwa Seleman Mzee amewataka wananchi wa Mtwara na Lindi kuchangamukia fursa hii. Vilevile amewataka wananchi kuzingatia sheria na taratibu za kuupokea mradi ili kusitokee vurugu zisizo na msingi.





No comments:

Post a Comment