MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205
Uzinduzi wa Mradi wa 'Tumani la Mama' katika Picha
Mradi wa Tumaini la Mama umezinduliwa mkoani Mtwara wiki hii katika uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara. Mradi huu unakusudia  kutoa huduma ya afya kwa wajawazito hadi mwaka mmoja baada ya kujifungua ambapo mama na mtoto wataipata huduma hiyo kupitia Bima ya Afya .
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu akikata utepe wa sanduku la huduma kwa wajawazito kama ishara ya kuzindua mpango huo ambao pamoja na mambo mengine, mjamzito anapewa vifaa vya kujifungulia mara tu anapowasili kliniki.
Waziri Ummy Mwalimu akimkabidhi mmoja wa wajawazito vifaa vya kujifungulia. Mpango huu utaondoa adha iliyokuwa ikiwapata akina mama sehemu mbalimbali hapa mkoani ya kutakiwa kununua vifaa vya kujifungulia mara tu wanapotakiwa kwenda hospitali kujifungua.

Mkurugenzi wa Benki ya watu wa Ujerumani (KFW),  Dr. Helmut Schoen akielezea malengo yaliyokusudiwa katika mradi huo kuwa ni pamoja na kuboresha huduma za upatikanaji wa tiba kwa familia za wanaMtwara na Lindi.
Mwakilishi toka ubalozi wa ujerumani, Mrs. Julia Hannig akiwasilisha ujumbe toka serikali ya Ujerumani. Ameeleza kuwa malengo ya mradi huo kuimarisha huduma za afya jambo ambalo serikali ya Ujerumani imekuwa ikifanya kwa muda mrefu na kwamba serikali hiyo bado iko tayari kushirikiana na serikali ya Tanzania kuhakikisha watanzania wote wanapata huduma ya Bima ya afya..
Wananchi wakifuatailia shughuli mbalimbali zinazoendelea katika uzinduzi wa mradi wa Tumaini la Mama katika Uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara..

No comments:

Post a Comment