MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Monday 30 March 2020

Polisi waimarisha ulinzi mpka wa Tanzania-Msumbiji







Jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya
ulinzi na usalama Vimeimarisha ulinzi katika mipaka ya Tanzania ili kuhakikisha
wahalifu wanaofanya mauaji na vurugu nchini Msumbiji hawapati nafasi ya kuingia
Tanzania. 

Hayo yamesemwa leo na Kamishna wa Operesheni na
Mafunzo wa Jeshi la Polisi Liberatus Sabas wakati akikagua kikosi maalumu cha
kupambana na uhalifu nchini kilichowasili mkoani Mtwara kwa ajili ya kuimarisha
ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Msumbiji. 
 
Amesema wahalifu hao wamekuwa wakivamia  kambi za jeshi, vituo vya polisi, kuchoma
moto na kuchukua silaha nchini Msumbiji na pia wameripotiwa kuvamia benki na
kupora fedha huko huko Msumbiji.

“Kule hali si shwali kama ambavyo mmekuwa mkisikia
kwenye vyombo mbalimbali vya habari. Sisi kwa kutambua hilo, na kutambua
umuhimu wa sisi kama Taifa, na umuhimu wa wananchi wa Tanzania kuwa shwali
tumejipanga kuhakikisha tatizo hili haliji huku kwetu.”

Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwasilisha
taarifa za mtu yeyote ambaye wanamtilia shaka.
 

No comments:

Post a Comment