Mpango wa serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha kila
mtanzania anapata Bima ya afya ambayo itamuwzesha kupata huduma ya matibabu
wakati wowote. Ili kufanikisha agizo hilo lililotolewa na Mhe Rais kwa Wizara ya Afya, Wizara imejipanga kuhakikisha mwaka 2019 inawafikia watanzania wote.
Picha
ya pamoja ya wafanyakazi wa NHIF mjini Mtwara na Naibu Waziri Mhe. Faustin
Ndugulile
“Kubwa ambalo serikali tumepanga
kulifanya mwaka huu ni kuhakikisha kila mtanzania anapata Bima ya Afya. Hili ni agizo la Mheshimiwa Rais kuhakikisha kila
mtanzania hahangaiki na huduma ya afya na badala yake atembee na kitambulisho
kinachomuwezesha kupata huduma hiyo.” Amesema Mhe. Ndugulile.
Amesema hadi sasa serikali imeendelea na maboresho katika
huduma mbamimbali za Bima ikiwemo CHF iliyoboreshwa inayomuwezesha mwanachama
kupata huduma ya afya kwenye vituo mbalimbali tofauti na ile ya awali ambayo
ilikuwa ikimuwezesha mwanachama kupata huduma kwenye kituo kimoja tu.
Pia huduma ya Ushirika Afya ambayo inalenga kuwafikia
wakulima walioko katika vyama vya ushirika vya mazao mbalimbali. Mheshimiwa
Naibu Waziri amempongeza ndugu Said Akili, mkulima wa korosho kutoka kijiji cha
Nyundo katika chama cha Msingi Nyundo B kwa kutambua umuhimu wa Ushirika Bima
na kujiunga. Aidha amesema Ushirika Bima inapatikana kwa shilingi 76,800 kwa
mwaka na inamuwezesha mwanachama kupata huduma ya afya kwenye vituo zaidi ya
elfu sita nchi nzima.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto Mhe. Faustin Ndugulile akimkabidhi Said Akili mwanachama wa chama cha
Msingi Nyundo B, kijiji cha Nyundo, Halmashauri ya Wilya ya Nanyamba kadi ya
uanachama wa Bima ya Afya (Ushirika
Afya) mara alipotembelea katika Ofisi za Bima ya Afya (NHIF) mjini Mtwara jana
Februali 26, 2019.
Amesema hizi huduma
zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza changamoto za huduma za afya. Kinachotakiwa
sasa ni kuhamasiha wananchi kujiunga na bima hizi kwani zitasaidia kwa kiasi
kikubwa kuondokana na changamoto hizi.
Kwa upande wake Said Akili amewataka wakulima wenzake
kuchangamukia huduma hiyo kwani changamoto za wakulima ni ninyingi.
“Wakulima wengi tunatumia jembe la mkono na Panga na tunakuwa
na fedha kipindi cha miezi ya mauzo. Baada ya hapo wengi tunakuwa hatuna fedha.
Bahati mbaya ugonjwa hauchaguai muda hivyo ukiwa na kadi ya Bima itasaidia
kupata huduma ya afya bila wasiwasi”. Amesema Said.
Naibu Waziri Mhe. Faustine Ndugulile akikagua taarifa mbalimbali
za huduma ya afya mara alipotembelea Hiospitali ya Rufaa ya Mkoa Ligula
Februali 26, 2019.
Mhe. Ndugulile amekuwa na zira ya siku mbili mkoani hapa
ambapo ametembelea maeneo mbalimblai ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Ligula,
Hospitali ya Kanda ya Kusini inayojengwa mjini Mtwara, Ofisi za Bandari Mtwara pamoja
na ofisi za Bima ya Afya Mtwara.
No comments:
Post a Comment