Msanga Mkuu Beach Festival ni sherehe maalumu ambayo itakuwa mara yake ya kwanza kufanyika mkoani Mtwara. sherehe hizi zitafanyika katika
beach ya MsangaMkuu Desemba 30 mwaka
huu huku ikitarajiwa kuwa na mwendelezo wa tukio la aina hii kila mwaka.
Muonekano wa Beach ya Msanga Mkuu kabla ya Kufanyiwa marekebisho
Sherehe hii inayosimamiwa na kamati maalumu iliyoundwa na Mkuu
wa Mkoa wa Mtwara ikishirikisha wadau kutoka taasisi za serikali, mashirika na
makampuni binafsi yanayofanya kazi zake mkoani Mtwara itahusisha mashindano ya michezo mbalimbali ngoma za asili, mieleka, kupiga mbizi, kupiga kasia, Soka la ufukweni, michezo ya watoto pamoja
na mingine mingi.
Wajumbe wa Kamati ya Maandalizi wakiwa eneo la tukio
Lengo la tukio hili ni kutangaza utamaduni, fursa za
kiuchumi, kitalii pamoja na kujenga mahusiano ya pamoja kwa wanaMtwara.
Wajumbe wa kamati ya Maandalizi wakikagua eneo linalozunguka Beach ya MsangaMkuu tayari kwa maandalizi ya tukio
Kamati ya Maandalizi ikijaribu usafiri wa kivuko cha ziada pamoja na vifaa vya usalama
No comments:
Post a Comment