Abiria wa Kivuko cha MV Mafanikio kinachofanya kazi zake kati ya MsangaMkuu na Mjini Mtwara wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa ndani ya kivuko hicho wakati alipokuwa akivuka kuelekea MsangaMkuu kwa lengo la kukagua hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya tamasha la MsangaMkuu Beach Festival linalotarajiwa kufanyika Desemba 29 hadi 30, 2018.
Wengi wa abiria wa kivuko hiki ni wafanyabiashara ndogondogo na MamaLishe hivyo walitumia fursa hiyo kuishukuru serikali kwa kuanzisha vitambulisho vya Ujasiliamali. Wamemuomba Mheshimiwa RC kuhakikisha wanavipata vitambulisho hivyo kwa haraka.
Kamati
ya Maandalizi ya tamasha la MsangaMkuu Beach Festival na Mkuu wa Mkoa
Mhe. Gelasius Byakanwa (wa sita kutoka kushoto) alipotembelea eneo hilo
Leo Desemba 19, 2018
Tamasha hili linatarajiwa kushirikisha
micheo mbalimbali ikiwemo mieleka, kupiga kasia, soka la ufukweni, ngoma
za asili, michezo ya watoto, mashindano ya kuimba, dansi na mingine
mingi
Picha
ya pamoja ya baadhi ya viongozi wa eneo la MsangaMkuu na Mkuu wa Mkoa
Mhe. Gelasius Byakanwa mara alipotembelea eneo hilo leo Desemba 19, 2018
kwa ajili ya kukagua hatua iliyofikiwa katika maandalzi ya tamasha la
MsangaMkuu Beach Festival linalotarajiwa kufanyika Desemba 29-30 katika
Beach hiyo.
Mhe. RC ameridhishwa na maandalizi na amewataka
wananchi wote wa mkoa wa Mtwara kushiriki naye katika kuufunga mwaka
2018 kwa tamasha hilo litakalokuwa likifanyika kwa mara ya kwanza mkoani
Hapa
Mkuu
wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa (wa tano toka kushoto) na
Watoa huduma wanaotarajiwa kuhudumia wageni mbalimbali watakaohudhuria
katika Tamasha la MsangaMkuu Beach Festival linalotarajiwa kufanyika
kuanzia Desemba 29 hadi 30 mwaka huu katika Beach ya MsangaMkuu.
Huduma zinazotarajiwa kuwepo ni pamoja na vinywaji vya aina mbalimbali, nyama choma, samaki wa kila aina, vyakula maalum kwa watoto na vingine vingi.
Huduma zinazotarajiwa kuwepo ni pamoja na vinywaji vya aina mbalimbali, nyama choma, samaki wa kila aina, vyakula maalum kwa watoto na vingine vingi.
Mkuu
wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akipata maelezo toka kwa
wajumbe wa kamati ya maandalizi ya tamasha la Msanga Mkuu Beach Festival
mara alipotembelea eneo linaloandaliwa kwa ajili ya tamasha hilo.
MsangaMkuu Beac Festival inatarajia kufanyika kuanzia tarehe 29-30, 2018 katika Beach ya MsangaMkuu
No comments:
Post a Comment