Mkuu
wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akiwa pamoja na Msanii Nassib Abdul
Maarufu kama Diamond Platinum wakati Msanii huyo pamoja na wasanii wenzake walipotembelea ofisni hapo katika ziara yao ya tamasha la Wasafi Festival linalotarajiwa kufanyika kesho Novemba 24, 2018
Picha ya pamoja ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius
Byakanwa na mama wa Msanii Nassib Abdul maarufu kama Diamond Platinum wakati
kundi la wasanii hao walipotembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa Novemba 23, 2018
MKuu
wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa akiwa na wasanii walioko katika ziara
ya tamasha la Wasafi. Kulia ni msanii Dudu Baya au Konki Master
Baadhi ya wasanii walioko katika ziara ya Tamasha la wasafi Festival linalotarajiwa kufanyika kesho Novemba 24, 2018.
Msanii Diamond Platinum akikabidhi fedha sh. 50,000 kwa mmoja
wa akina mama.
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa amemshauri Msanii Nassib Abdul maarufu kama Diamond Platinum pamoja na wasanii kujenga chuo cha Sanaa mkoani Mtwara. Amesema Mkoa wa Mtwara una vipaji
vingi vya sanaa lakini hakuna chuo cha kuweza kuwaandaa kitaaluma.
Mheshimiwa Byakanwa ameyasema hayo leo wakati alipotembelewa
na kikundi cha wasanii cha Wasafi ambacho kinatarajia kufanya tamasha la
burudani kesho Novemba 24, 2018 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona ulioko Mjini
Mtwara.
Amesema sanaa ni ajira, sanaa ni fursa, sanaa ni nafasi ya
kujikomboa kimaisha lakini ina muda wake ambao msanii anatakiwa kujiandaa ili
wakati huo ukifika awe na njia mbadala ya kuendeleza maisha.
Mtwara kuna waigizaji
wengi, kuna wasanii wengi na watu wa Mtwara wanapenda sanaa. lakini kama taifa
tuna vyuo vichache sana vinavyoweza kuzalisha wasanii… tunawea kuwa na taasii
ambayo tunaweza kuzalisha wasanii wengi na vipaji vingi zaidi. hizo ni fursa
ambazo zipo. Mnaweza kuzitumia kwa pesa mnazozipata kwa kipindi hiki. Amesema
Byakanwa.
Mheshimiwa Byakanwa amewashukuru wasanii wote wakiongozwa na
Msanii Nassib Abdul maarufu kama Diamond Platinum kwa kuchagua kuja Mtwara. Pia
ameshukuru kwa msaada walioutoa kwa makundi mbalibmlai katika jamiii ambao ni
pikipiki tatu ambazo wameelekeza ziende kwa shule tatu zinazofanya vizuri
katika mitihani ya kitaifa, milioni tano ambazo zilimetolewa kwa akina mama mia
moja ambapo kila mmoja alikabidhiwa shilingi 50,000, sare za shule pea 100 kwa
wanafunzi 100 pamoja na madaftari, kalam penseli pamoja na vitabu.
Akizungumzia msada walioutoa, Msanii Diamond Pratinum
ameshukuru uongozi wa Mkoa wa Mtwara kwa mapokezi mazuri waliyoyapata. Amesema
msaada huo ni kutokana na kuguswa na hali duni ya maisha kwa jamii ya
kitanzania.
Amesema msaada huo haujatoka kwa wasafi peke yao bali ni
kundi zima la wasanii waliombatana pamoja kuja Mtwara,
kwa upande wake Msanii Dudu baya ameshukuru serikali zote
zilizotangulia. Amesema yako maendeleo ambayo wengine wanajifanya hawayaoni
wakati yako wazi. Ametolea mfano kuwa miaka ya 2005 barabara ya kuja Mtwara ilikuwa
ya vumbi ambapo yeye mwenyewe aliwahi kusafiri na kufika Mtwara akiwa amejaa
vumbi hadi masikioni, lakini safari hii amesafiri kwa lami tangu Dar es Salaam
hadi Mtwara akiwa katika hali yake ya kawaida ya usafi. Amesema hiyo ni hatua
kubwa ya maendeleo kwa Tanzania.
Kikundi cha wasafi kinachojumuisha wanamziki na waigizaji maarufu
hapa nchini wako Mtwara kwa ajili ya kufanya tamasha maalumu linalojulikana
kama wasafi Festival ambalo litafanyika kesho kwenye uwanja wa Nangwanda
sijaona kuanzia saa 12 jioni.
No comments:
Post a Comment