Nyumba za watumishi wa zahanati ya Imekuwa halmashauri ya Wilaya ya Mtwara zilizojengwa na Benjamin Mkapa Foundation
Zahanati ya Kawawa
Ellen Mkondya Senkoro. Mkurugenzi Mtendaji Benjamin Mkapa Foundation
Mganga Mfawidhi, Zahanati ya Kawawa, Hadija Marekana
Taasisi ya Benjamin Mkapa imejenga jumla ya nyumba 50 za
watumishi wa Afya mkoani Mtwara. nyumba hizo zimejengwa katika zahanati na
vituo vya afya sehemu mbalimbali mkoani hapa huku zikigharimu taribani milioni
53 hadi 68 kila nyumba.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa nyumba hizo zilizojengwa
kati ya mwaka 2011 na 2015 Mkurugenzi Mtendaji Benjamin Mkapa Foundation Dkt.
Ellen Mkondya Senkoro amesema waliamua
kufanya hivyo kutokana na mahitaji makubwa ya nchi na wamejenga jumla nyumba 480 nchi nzima.
Amesema ujenzi huo ulizingatia vituo ambavyo vilikuwa
havifanyai kazi kutokana na changamoto ya nyumba za watumishi na hivyo
kuwezesha kufanya kazi na kusaidia kwa kiasi kikubwa huduma kwa jamii.
Kwa upande wake Mganga Mfawidhi Hadija Marekana wa Zahanati
ya Kawawa pamoja Joseph Sheduo wa zahanati ya Imekuwa kwa nyakati tofauti
wameshukuru taasisi hiyo kwa msaada huo na kwamba imesaidia kwa kiasi kikubwa
kuondoa tatizo la huduma ya afya kwa jamii.
Wamesema kabla ya ujenzi wa nyumba katika zahanati hizo walikuwa wakilazimika kusafiri kutoka vijiji
jirani kwenye makazi yao jambo ambalo lilikuwa likikwamisha huduma za haraka
hasa nyakati za usiku.
Kwa upande wake Fatuma Selemani wa kijiji cha Imekuwa anasema
wamepata ahueni kubwa baada ya ujenzi wa nyumba hizo kwani hata usiku wa manane
wanawaamusha waganga na kupata huduma.
No comments:
Post a Comment