Balozi
wa Nigeria nchini Tanzania DKt. Sahabi Issa Gada akisaini kitabu cha wageni.
Mhe. Byakanwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akizungumza na Mgeni
wake, Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Dkt. Gada
Dkt. Gada akionesha ramani ya Nigeria inayoonesha fursa mbalimbali za kiuchumi
Dkt. Gada akikabidhi tuzo yenye nembo ya serikali ya Nigeria kama kumbukumbu ya ziara yake kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa amekutana
na kufanya mazungumzo na Balozi wa Nigeria nchini Tanzania DKt. Sahabi Issa
Gada ofisini kwake.
Dr. Gada aliyeambatana na Uongozi wa Kiwanda cha saruji cha Dangote
Pamoja na Maafisa wa ubalozi huo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli pamoja na uongozi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
kwa jitihada kubwa wanazofanya kuhakikisha uwekezaji uliofanywa na Alhaji Aliko
Dangote, raia wa Nigeria, katika kiwanda cha saruji cha Dangote unaendelea
vizuri.
Amesema serikali ya Nigeria ina imani kubwa na serikali ya
Tanzania na kwamba wataendelezaa mahusiano hayo.
Aidha Dkt. Gada amemkabidhi Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ramani ya
Nigeria kuonyeha maaeneo mbalimbali ya fursa za kiuchumi na kusema Nigeria inazo
fursa nyingi za kiuchumi ambazo wanaweza kushirikiana na serikali ya Tanzania.
No comments:
Post a Comment