Serikali kupitia mradi wa uendelezaji miji Mkakati (Tanzania Strategic
Cities Project) imetoa bilioni 21.7 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu
mbalimblai ya maendeleo katika Manispaa ya Mtwara mikindani. Miradi hiyo ni
pamoja na ujenzi Wa barabara 4 za mitaa kwa kiwango cha lami, Ujenzi wa maeneo
matatu ya kupumzikia (Recreation Center), mfereji mkubwa wa kuondoa maji ya
mvua, ujenzi wa soko la kisasa pamoja na kituo cha daladala eneo la Mikindani.
Akizungumza leo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo iliyofanywa
na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda amesema
fedha hizo zimetolewa kwa mkopo na Benki ya dunia na kwamba ujenzi wa miradi
hiyo yote inatarajiwa kukamilika ifikapo oktoba 2019.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa amesema kukamilika kwa
miradi hiyo kutaufanya mji wa mtwara kuwa na muonekano mzuri na kwamba hiyo
ndiyo hatua nzuri kuifanya Manispaa kuwa na sifa ya kuwa jiji.
“Naamini baada ya
kukamilika miradi hii Mtwara itakuwa sehemu nyingine na pengine inaweza kupata
sifa ya kuelekea kuwa jiji”.
Amewataka vijana waliopata nafasi ya kuajiliwa katika ujenzi
wa miundombinu hiyo kuwa waamifu ili kujijengea imani kwa waajili.
No comments:
Post a Comment