MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Monday 20 August 2018

kikao cha wadau wa elimu Mtwara Agosti 20, 2018

Ni katika kuendeleza jitihada za kuleta mageuzi chanya ya elimu Mkoani Mtwara. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imeitisha kikao chenye lengo la kutathimini tulikotoka na tunakoelekea katika kuleta mageuzi chanya ya elimu mkoani Mtwara.

Kikao hicho kilitanguliwa na ziara ya wadau ambao walitokea sehemu mbalimbali mkoani hapa kutembelea vituo mbalimbali kwa lengo la kuangalia nini kinafanyika katika kuleta maendeleo katika sekta ya elimu. wadau walitembelea Shule ya Msingi Mbuo ambako walijifunza njia rahisi ya kuwafundisha watoto wa awali kupitia madarasa yanayoongea ambayo yamefadhiliwa na mradi wa Tusome Pamoja. Pia wamejifunza juu ya ushiriki wa jamii na walimu katika suala zima la ufundishaji na ujifunzaji.

Shule ya msingi Kambarage walijifunza juu ya Umoja wa Walimu na Wazazi (UWAWA) na Umoja wa Walimu na Jamii (UWAJI) jinsi wanavyotekeleza shughuli zao kwa pamoja.

Chuo cha ufundi VETA walishuhudia jinsi VETA inavyosaidia kuendeleza wanafunzi wanaomaliza shule za msingi na sekondari na jinsi wanavyo wawezesha kupata stadi za maisha. 

Mtwara Kawaida kulikuwa na maarifa ya walimu wanavyoandaliwa katika hatua mbalimbali na changamoto wanazokutana nazo katika kufikia azima ya kuwapata walimu bora.

No comments:

Post a Comment