Kituo hiki kimekuwa kikifanya kazi katika mazingira magumu
kutokana na tatizo la gari la usafiri kwa wafanyakazi hali ambayo imekuwa
ikisababisha usumbufu katika suala la ulinzi na ukusanyaji wa mapato.
“Kituo chetu cha forodha hakina gari na mpaka wetu ndio hivi
uko wazi kabisa, wananchi wanatembea, wanakatiza hapa mtoni, kwa hiyo udhibiti
kiusalama, kimapato unakuwa mgumu sana. Tumekubaliana na viongozi wa mamlaka ya
mapato kwamba kabla ya tarehe 15 mwezi wa tisa wawe wameleta gari kwa ajili ya
kuhudumia kituo hiki”.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalma
Wilaya ya Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda
amemshukuru Mheshimiwa Waziri. Amesema muingiliano wa watu wa Mtwara na
Msumbiji ni mkubwa kwa sababu ni watu wa jamii moja, kabila moja na dini moja. Amesema
kwa hali kama hiyo ni rahisi mtu mwenye nia mbaya kujipenyeza. Hata hivyo bado
ulinzi wa mpaka umeimarika
“Hatujawa na tatizo na ndio maana tunajivuna kwamba Mtwara
iko shwari. Tunazungumza kwa kifua mbele kwamba wenye kuja waje. Mtwara iko
salama Mtwara ni mahali pazuri panakalika.” Amesema Mmanda.
No comments:
Post a Comment