Jenifer Elasto. akipokea zawadi ya Mshindi wa kwanza katika mpira wa volleyball kwa niaba ya wenzake kanda ya Nanyumbu = Masasi.
Akizungumzia maandalizi kupitia mchezo wa volleybal ambao umekuwa ukifanya vema ngazi ya Taifa Jenipher Elasto, kidato cha tatu shule ya Sekondari Mangaka amesema hana wasiwasi na ushindi wa kwanza kwani wameandaliwa vizuri. Kwa upande wake Msham Sadiki kutoka Newala amesema kikosi cha mwaka huu kina ari zaid kuliko miaka yote hivyo hana mashaka na ushindi. wote kwa pamoja wamewataka wanaMtwara kuwaombea ili wafanye kile walichoandaliwa
Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara Alfred Luanda akikabidhi kombe la Mshindi wa Jumla kwaMwakilishi wa Kanda ya Tandahimba - Newala
Akikabidhi vikombe kwa washindi. Mgeni Rasmi, Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara Alfred Luanda amewataka wanafunzi wote waliochaguliwa kuhakikisha wanawakillisha vema mkoa katika ngazi ya Taifa. Amesema mara nyingi wanamichezo wa kitanzania wamekuwa wakishindwa kufanya vizuri kutokana na kutojiamini hivyo wao wanapaswa kuepukana na hali hiyo.
·
Washindi wa Jumla mashindano ya UMISETA ngazi ya
mkoa Mtwara Kanda ya Tandahimba-Newala wakifuatilia hotuba toka kwa Mgeni Rasmi
Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, ALfred Luanda (hayupo pichani) wakati wa kilele
cha mashindano hayo Mei 31, 2018 yaliyofanyika uwanja wa Chuo cha Ualimu Mtwara
(K). Pamoja na kikombe cha Ushindi wa Jumla washindi hao wamekuwa wa kwanza
katika michezo ya Riadha wavulana na wasichana na mpira wa mikono kwa
wasichana.
Vikombe vinne vilivyochukuliwa na kanda ya Mtwara - Nanyamba ambavyo ni Mpira wa mikono wavulana, mpira wa kikapu wavulana na wasicha, mpira wa wavu (netball) na mpira wa miguu wavulana.
Vikombe vitatu vilivyochukuliwa na Kanda ya Masasi -
Nanyumbu ambavyo ni Mpira wa wavu wavulana na wasichana na mpira wa
miguu wavulana.
Kanda zingine zilizokuwa zikiunda mkoa wa Mtwara ni kanda ya Masasi na Nanyumbu na kanda ya Mtwara na Nayamba. kilele cha mashindano haya kitaifa ni tarehe 15 Juni 2018 mjini Mwanza.
No comments:
Post a Comment