MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Saturday 28 April 2018

TET watakiwa kusimamia maudhui



Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mheshimiwa Evod Mmanda ameitaka Taasisi ya Elimu ya Tanzania (TET) kuhakikisha inasimamia maudhui katika vitabu vinavyozalishwa ili yalenge matakwa ya jamii ya watanzania. Amesema vitabu vinahifadhi maarifa ambayo ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa lolote duniani hivyo usimamizi imara wa maudhui yanayowekwa kwenye vitabu ni muhim kwa maendeleo ya Taifa


Mheshimiwa Mmanda ameyasema hayo leo wakati akipokea vitabu vilivyotolewa na Tasisi ya Elimu Tanzania (TET) kwa mkoa wa Mtwara katika hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Ufundi Mtwara.

Amesema hana mashaka na kazi ya Taasisi ya Elimu Tanzania kutokana na weledi wanaouonesha katika kusimamia kazi zao hivyo moyo huo unapaswa kuendelea ili kuzalisha taifa la wazalendo.

Akizungumzia juu ya mapokezi ya vitabu hivyo Mheshimiwa Mmanda ameshukuru serikali ya awamu ya tano kwa kuwa na nia ya dhati ya kulifikisha taifa katika malengo yaliyokusudiwa. Amesema serikali ya awamu ya tano tangu ilipoingia madarakani ililenga kuhakikisha kila mwanafunzi anakuwa na kitabu cha kujifunzia na azima hiyo imefikiwa. Ametoa wito kwa walimu wahakikishe wanavitumia badala ya kuvifungua ofisini. 
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Elimu Tanzania, Profesa Benadeta Kiliani amesema zoezi la usambazji wa vitabu Tanzania Bara lilianza mwezi Februali mwaka huu na limekuwa likienda vizuri.


Amezitaka halmashauri zote zilizokwisha pokea vitabu hivyo wavisambaze haraka shuleni hatimaye kwa wanafunzi ambao ndio walengwa. 

Amevitaja vitabu vinavyosambazwa kuwa ni vitavu vya kiada na kuanzia darasa la kwanza hadi la Nne. Pia kiongozi cha Mwalimu. Hadi Februali 27 mwaka huu walikuwa wamesambaza vitabu vya darasa la kwanza hadi la tatu kwa mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Tanga, Dodoma, Singida, Manyara Arusha na Mwanza. Aidha kati ya April 29 hadi Mei 5 mwaka huu watakuwa wameifikia mikoa ya  Simiyu, Shinyanga, Pwani na Mara.


Akizunguza kwa niaba ya Maafisa Elimu Mkoa wa Mtwara, Afisa Elimu Msingi, Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, Said Farahani amesema uamuzi wa serikali kusambaza vitabu hivyo ni mzuri. Amesema hiyo ndiyo njia sahihi ya kulifikisha taifa katika maendeleo yaliyokusudiwa.

No comments:

Post a Comment