Akizungumza na waandishi wa
habari leo mjini Dodoma, mazunguzo ambayo video yake inapatikana kwa kubonyeza
HAPA, Mheshimiwa Dr. Tizeba amesema amemuagiza Katibu Mkuu achukuwe hatua hiyo
kuanzia leo Aprili 21, 2018 na kwamba taratibu za kumpata atakayekaimu nafasi
hiyo zitafanyika ndani ya kipindi kifupi.
‘Baada ya kuangalia mwenendio na
kutafakari zao la korosho linavyokwenda, upatikaji wa viwatilifu, kwa ujumla
linavyosimamiwa, nimeamua kuchukua hatua ya kusitisha mkataba wa aliyekuwa Mtendaji
Mkuu wa Bodi ya Korosho Bwana Hassan Jaruf kama Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya korosho’.
Amesema Tizeba
Kwa muda mrefu sasa Bodi ya
Korosho imekuwa ikilalamikiwa kutokana na kasoro mbalimbali za usimamizi wa zao
hilo. katika musim wa 2017/2018 Bodi ya Koroho ililalamikiwa kwa kuchelewesha
magunia ya kuhifadhia korosho jambo ambalo lilimsukuma Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
Mheshimiwa Gelasius Byakanwa kuunda Tume kubaini chanzo cha kasoro. Tume hiyo
ilibaini kuwepo mapungufu ambayo yalisabishwa na kutokuwajibika kwa Bodi ya
Korosho.
Aidha katika msimu wa mwaka huu
2018/2019 Bodi ya Korosho imeendelea kulalamikiwa kwa kuchelewesha pembejeo.
No comments:
Post a Comment