DIwani wa kata ya Makonga wilayani Newala Mussa Makungwa amehama kutoka Chama cha Wananchi CUF na kujiunga na Chama cha mapinduzi. Uamuzi huo ameufanya wiki hii wakati wa ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu aliyoifanya Wilayani hapo.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa Yusuph Said Nannila akimkabidhi Kadi ya CCM Diwani wa kata ya Makonga Mussa Makungwa mara baada ya kutangaza kujitoa CUF na kuhamia CCM
Akitangaza kukihama chama hicho Makungwa amesema ameamua kufanya hivyo ili kuungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Magufuli katika jitihada za kuwaletea maendeleo watanzania.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mtwara Yusuf Said nannila amemshukuru Diwani huyo kwa kufanya uamuzi sahihi na kuwataka wananchi watu wengine kuiga mfano wake
No comments:
Post a Comment