MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Tuesday 6 December 2016

Vietnum Wakanusha Korosho Kukwama Mtwara



Wakati vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini vikiripoti kukwama kwa shehena ya korosho tani 3800 katika bandari ya mtwara, wafanya bishara wa Vietnum, kampuni za Starnut na Diaoune Et Freres LTD zilizoripotiwa kutoa taarifa hiyo zimekanusha kuwa hawajakumbwa na tatizo la aina hiyo na kwamba wamepata ushirikiano wa hali ya juu toka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara. 
 
Akizungumza na vyombo vya habari katika Hotel ya La ville Novel Mkoani hapa, mwakilishiwa kampuni hizo mbili Omega Mnali amesema walioripoti taarifa hizo walikuwa na makusudi yao binafsi tofauti na ukweli ulivyo.
Amesema shehena iliyoripotiwa na kiasi cha tani 3800 siyo kweli . Anasema mara baada ya kuwasili hapa nchini kwa ajili ya kunua korosho walifanya mawasilianio na kampuni moja kubwa ya ‘clearing and forwarding ya jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusafirisha mzigo.
Waliendelea kuwasiliana na kampuni hiyo juu ya changamoto wanazokutana nazo katika usafirishaji ikiwa ni pamoja na tatizo la kupata makasha ya kubebea korosho kutoka kampuni ya PIL inayotoa huduma hiyo. Anaendelea kuwa awali waliingia mashaka ya kuwepo na upendeleo toka IPL katika utoaji wa makasha.
Hata hivyo hawakulalamika kwenye vyomba vya habari badala yake walilipoti kwenye uongozi wa mkoa kwa ajili ya kupata msaada jambo ambalo llilifanyiwa kazi kwa muda mfupi.
Omega aliendelea kuwa inawezekana kampuni hiyo iliyokosa kazi baada ya kuelezwa miongozo iliyoko mkoani hapa kuwa korosho haitaweza kupita Dar es salaam jambo ambalo liliwafanya wawasiliane na vyombo vya habari ili kushinikiza serikali kubadili maagizo.
Anaendeeal kuwa kampuni zote mbili zimepata ushirikinao wa hali ya juu kutoka mkoani na kwamba wanamatumaini ya kupata masaada zaidi tofauti na ilivyoripotiwa.
Alitaja kiasi cha makasha waliyokwisha safirisha kuwa Kampuni ya Starnut imeshasafirisha makasha 96 wakati kampuni ya Diaoune Et Freres LTD ilikuwa imesafirisha makasha 12. 
Omega anawaomba wananchi na watanzania kwa ujumla kuzipuuza taarifa hizo na kuwaomba radhi wote walioguswa na taarifa hizo.

Tazama video yote hapa.

 

No comments:

Post a Comment