MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Wednesday 7 December 2016

Malaysia kuwekeza Mtwara.



1kikao cha majadiliano kati ya DESA 7 na wajumbe wa Sekretarieti ya mkoa. kutoka kulia ni Rais wa Desa 7, Safrudin Mahfoz. Makamu wa Rais wa Desa 7   Zulkifli Saldad, Mkurugenzi mtendaji wa kampuni,  Isiaka Katundu pamoja na International Business Development (executive),Salim Maliwanga. mwenyekiti wa kikao ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Dr. Khatib malimi Kazungu




Wakati mkoa wa Mtwara ukiwa katika maandalizi ya kongamano la uwekezaji linalotarajiwa kufanyika mapema mwezi Januari, 2017, ishara njema ya mvuto kwa wawekezaji imeanza kuonekana. Moja ya wageni walioonesha nia ya kuwekeza katika viwanda ni pamoja na kampuni ya DESA 7 Resources yenye makao yake nchini Malaysia.

Akizungumza na Kaimu Mkuu wa  Mkoa wa Mtwara, Khatib Malimi Kazungu mapema asubuhi leo, Rais wa kampuni hiyo, Safrudin Mahfoz amesema amevutiwa kuwekeza katika kiwanda cha kuhudumia makampuni yanayoshughulika na utafiti wa Mafuta na gesi Mkoani hapa.

Amesema kampuni yake inashughulika na kazi nyingi lakini kubwa lililowavutia mkoani Mtwara ni kutengeneza na kukarabati vifaa vinavyotumika katika uchimbaji  na utafiti wa mafuta na gesi (Tubular and drilling Inspection and maintenance). 
Akielezea juu ya uzoefu wake nchini Tanzania amesema tangu kazi za utafiti na uchimbaji wa mafuta na Gesi nchini imeanza vifaa hivi vimekuwa vikiagizwa kutoka ulaya. Aidha hata pale ambapo vimekuwa vinahitaji matengenezo vimekuwa vikipelekwa Ulaya.
Kwa kufungua kiwanda hicho hapa Mtwara kutasaidia kuondoa usumbufu na kusogeza bidhaa karibu na hivyo kukuza uchumi wa nchi. 
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Isiaka Katundu amesema endapo kiwanda hiki kitajengwa, kitaajili watanzania zaidi ya 250 na kuwezesha  mafunzo kwa watanzania katika teknolojia hii na hivyo kuongeza fursa ya ajira mkoani hapa.
Mapema akielezea fursa za uwekezaji mkoani hapa, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mheshimiwa Dr. Khatib Malimi Kazungu amesema Mtwara ni eneo sahihi la kuwekeza na kwamba zipo fursa nyingi za uwekezaji zikiwemo viwanda vya kusindika samaki, mazao ya vyakula na kubangua korosho.
Dr. Kazungu ambaye kitaaluma ni Mchumi amesema mkoa uko tayari kutoa ushirikiano wa kila hali kuhakikisha wawekezaji wanapata mazingira mazuri ya kufanya kazi zao. Aidha amewataka watu wengine wenye nia ya kuwekeza mkoani mtwara waje
picha ya pamoja ya wajumbe wa Sekretarieti ya mkoa na viongozi wa DESA 7






       

No comments:

Post a Comment