Sijawa
Omary, Mtwara
VITENDO
vya kulawiti watoto wadogo wa
kiume kinyume na maumbile wenye umri wa kuanzia miaka 3 hadi 12 vimekuwa
vikiongezeka katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara.
Hayo
yamebainishwa hivi karibuni na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Lucas Mkondya
wakati alipokuwa akitoa taarifa hiyo mbele ya waandishi kutoka vyombo
mbalimbali vya habari mkoani hapa.
Amesema
kuwa, vitendo hivyo kwenye halmashauri hiyo vimekuwa vikiongezeka kuanzia mwezi
August hadi Oktoba mwaka huu ambapo jumla ya matukio 11 yameripotiwa kituoni
hapo.
Ameyataja
maeneo ambayo watoto hao wamekuwa wakifanyiwa vitendo hivyo viovu kuwa ni
pamoja na sehemu za mafundisho ya dini, shuleni na majumbani.
“Vitendo hivi vinavyoendelea katika jamii zetu ni kinyume na
taratibu na ni ukiukwaji wa sheria, lakini pia kutowatendea haki watoto
hawa ni udharirishaji“,Alisema Mkondya
Ameongeza
kuwa kumfanyia mtoto vitendo kama hivyo ni kumsababishia matatizo ya kiafya madhara
mbalimbali ya kimwili.
Amesema
Jeshi hilo tayari limewafikisha mahakamani watu wawili na linaendelea na
uchunguzi wa matukio mengine kadhaa ya aina hiyo.
Hata
hivyo Kamanda huyo ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwaangalia watoto wao kwa
kuwa makini pindi wanaporudi toka maeneo hayo ya dini na shuleni ili kubaini
usalama wa mtoto na kuhakikisha hawalali kitanda kimoja na msichana au mvulana
wa kazi (house girl/boy).
“Tatizo
linakuja kutokana na wazazi au walezi kupenda kumlaza msichana wa kazi au
mvulana wa kazi na mtoto mdogo kitanda kimoja sasa niombe tu jamii au
wanamtwara, hii tabia muiache mara moja ili kulinda usalama wa watoto
wetu”,Alisema Mkondya.
Vilevile
amesema jamii inapaswa kuwandalia mazingira mazuri watoto ili kuondokana na
vitendao hivyo viovu vinavyondelea katika halmashauri hiyo ili kulinda usalama
wa watoto hao.
Wakazi
katika halmashauri hiyo wametoa maoni yao juu ya vitendo hivyo huku baadhi
yao wakilaani wale wote ambao wamekuwa wakijihusisha na vitendo hivyo kwa
watoto hao.
“Maoni
yangu mimi kama mkazi wa Mtwara ni kutowafumbia macho wote waliohusika na
vitendo hivyo. Lazima sheria ichukuliwe mkondo wake dhidi yao ili iwe mfano kwa
wengine”,Alisema Edgar Mertusi
Veronica
Peter ameiomba mamlaka husika kuwachukulia hatua kali za kisheria watu
watakaobainika wanafanya vitendo hivyo na kulaani vikali kwani ni moja ya
udharirishaji na kutowatendea haki pia ukiukwaji wa haki za binadamu.
Hata
hivyo amesema kuwa, hata katika maandiko ya dini vitendo hivyo vimekuwa
vikilaaniwa na kukatazwa. kwani vimekuwa vikimdharirisha mtoto au binadamu na
kumfanya ajione hana tena thamani katika jamii sanjali na kumletea athari kubwa
kisaikolojia.
Kufuatia
hali hiyo jeshi hilo limepanga kufanya operesheni na misako ili kubaini maeneo
yote hatarishi ili kuweza kukomesha vitendo hivyo ambavyo vinaonekana kushamiri
hapa mkoani hapa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment