Ubora wa Bandari ya Mtwara umeendelea
kuonekana huku Zanzibar ikitafakari uwezekano wa kuitumia bandari hiyo
kusafirisha mafuta. Hiyo inatokana na maboresho yanayoendelea katika bandari
hiyo ikiwemo ujenzi wa Gati mpya yenye urefu wa mita 300 na kina cha mita 14.
Mwalimu Alli Mwalimu
Akizungumza na mwandishi wetu leo
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Maji na Nishati Zanzibar (ZURA), Mwalim
Alli Mwalim amesema yeye pamoja na Bodi nzima ya ZURA wameamua kutembelea mkoa
wa Mtwara ili kujifunza mambo mbalimbali ikiwemo fursa ya matumizi ya Bandari
hiyo katika kusafirisha mafuta kutoka nje ya Nchi.
Amesema kwa sasa wanaitumia sana
Bandari ya Dar es Salaam lakini wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali
ikiwemo kusubiri kwa muda mrefu kupakua mzigo hali ambayo imekuwa haiwapendezi
wafanyabiashara.
Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Maji na Nishati
Zanzibar (ZURA) wakipata maelezo juu ya Bandari ya Mtwara mara baada ya
kuitembelea Bandari hiyo leo
Mbali na Bandari ya Mtwara Bodi
hiyo ambayo itakuwa na ziara ya siku mbili Mkoani hapa itatembelea Kiwanda cha
Saruji kcha Dangote, Kituo cha uzalishaji wa Nishati ya Umeme cha Mtwara,
Kiwanda cha Kuchakata Gesi Asilia Madimba pamoja na visima vya Gesi asilia
vilivyoko Pwani ya Mnazi.
Amesema yako mengi yanayowavutia kujifunza
kutoka Mtwara hasa ikizingatiwa kuwa Mamlaka ya Udhibiti wa Maji na Nishati Zanzibar
haina muda mrefu tangu imeanzishwa hivyo wanahitaji muda wa kujifunza kutoka
sehemu mbalimbal nchini.
Nelson Cosmas Mlali. Mkuu wa Bandari ya Mtwara
Awali akiwasilisha taarifa ya hali
ya Bandari ya Mtwara, Mkuu wa Bandari hiyo Nelson Cosmas Mlali amesema
maandalizi ya kuanza kusafirisha mafuta kupitia Bandari ya Mtwara ziko katika
hatu ya mwisho. Lengo ni kuifanya Mtwara kuwa kituo cha kuhudumia mafuta kwa mikoa
ya kusini.
Baadhi ya maboresho yanayoendelea
hapo ni pamoja na ujenzi wa gati mpya yenye urefu wa mita 300 na kina cha mita
14. Aidha baada ya maboresho hayo bandari itakuwa na uwezo wa kuhudumia shehema
ya tani 600,000 toka 400,000 za sasa.
Cosmas Komba, Kaimu Katibu
Tawala Msaidizi Huduma za Maji na Nishati mkoa wa Mtwara
Kwa upande wake Kaimu Katibu
Tawala Msaidizi anayehughulikia Huduma za Maji na Nishati mkoa wa Mtwara Cosmas
Komba ameshukuru ujio wa wageni hao akielezea kuwa ni fursa nzuri ya wageni
kujifunza mambo mbalimbali yanayoendelea mkoani Mtwara. amesema Mkoa unazo
fursa nyingi ambazo ziko wazi kwa kila mwananchi hivyo wote wanaalikwa.
No comments:
Post a Comment