Bandari ya Mtwara
imeendelea kuonesha uwezo mkubwa wa kutoa huduma baada ya kupokea meli yenye
urefu wa mita 200 sawa na viwanja viwili vya mpira. Meli hiyo iliyoleta malori
651 ya kampuni ya Dangote inayozalisha saruji mkoani hapa ilitia nanga bandari
ya Mtwara jana saa 10:30 jioni ikitokea nchi za Mashariki ya Mbali.
Akizungumza baada ya
mapokezi ya meli hiyo Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Dr. Khatib Malimi
Kazungu amesema hiyo ni ishara kwa watanzania na dunia nzima kuwa Bandari ya
Mtwara ina uwezo mkubwa katika kuhudumia meli za aina yoyote.
Amesema watanzania
wanapaswa kuachana na porojo za mtaani ambazo zimekuwa zikiwataka
waamini kuwa bandari ya Dar es Salaam ndiyo yenye uwezo tu.
Kwa upande wake Meneja utekelezaji
kampuni ya Diamond Shipping iliyosimamia kuja kwa meli hiyo, John Lemomo amesema
meli hiyo yenye uwezo wa kubeba magari 6500 ni ya kisasa kabisa na ina ghoraja
13 ambapo 12 kati yake ni kwa ajili ya kubeba mizigo Wakati ghorofa ya mwisho
ni kwa ajili ya huduma ya malazi, chakula na ‘control room’
Amesema pamoja na malori
651 ya Dangote meli hiyo imebeba magari 700 yanayoenda kushushwa Dar es Salaam,
na mengine zaidi ya 2000 yanapelekwa Kenya.
Meneja
utekelezaji kampuni ya Diamond Shipping Company LTD, John Lemomo, akizungumza
na waandishi wa Habari (hawapo pichani)
Lemomo amesema kabla ya
kuamua kuileta meli hiyo hapa Mtwara walijiuliza maswali mengi hasa juu ya
uwezo wa bandari hiyo kupokea meli ya aina hiyo. Baada ya mawasilianio na
vielelezo vya kitaalamu kutoka pande zote mbili waliamini kuwa inawezekana
hivyo wakaamua kufanya hivyo, jambo ambalo kweli limewezekana.
Kwa upande wake Katibu
Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda amesema huu ni muda wa wananchi kubadili
mtazamo. Kama ilivyozoeleka hapo zamani kuona mizigo ikitoka Dar es salaam kuja
Mtwara, leo dunia ikubali mageuzi haya kuwa sasa ni muda wa Dar es Salaam
kuiona mizigo ikitokea Mtwara kwenda kwenda huko.
Mapinduzi ya ujio wa
viwanda Mtwara inawezekana na mazingira yote ya kuruhusu hali hiyo
yameandaliwa. ‘Alisisitiza’
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Alfred Luanda akizungumza na wageni waliokuja kushuhudia tukio.
Wakati meli hiyo ikitua bandarini hapo, shangwe na nderemo zilisikika toka kwa wananchi wa mkoa wa Mtwara. Akielezea furaha yake, Flora
Millinga mkazi wa Mtwara amesema furaha yake imechanganyika na mambo mawili makuu. Kwanza
meli hiyo imeidhihirishia dunia kuwa Bandari ya Mtwara ni bora na ina uwezo
mkubwa katika kuhudumia meli za aina yoyote.
Aidha tukio hilo pia
limezima kelele za watu walioanza kueneza uvumi kuwa Dangote atafunga kiwanda
chake na kuhamia Kenya.
Kutua kwa meli hiyo kumekuja wakati mmiliki wa Kiwanda cha Dangote, Alhaji Aliko Dangote akiwa ametoa maelezo yenye kusisitiza kuwa ana matumaini na Tanzania. Ana matumaini na kiwanda chake cha Saruji kilichoko hapa Mtwara hivyo hana ndoto tofauti na kuwekeza zaidi nchini Tanzania.
Maelezo hayo pamoja na tukio la kushusha magari hayo inazima ndoto za sintofahamu iliyotawala kwa muda kadhaa hapa nchini kuwa atakifunga kiwanda hicho.
Maelezo hayo pamoja na tukio la kushusha magari hayo inazima ndoto za sintofahamu iliyotawala kwa muda kadhaa hapa nchini kuwa atakifunga kiwanda hicho.
Wananchi wa mkoa wa Mtwara wakiwa eneo la Bandari tayari kushuhudia tukio la Meli yenye malori ya Dangote kutia nanga bandarini hapo.
Naona Mtwara kuchele kazi nzuri Kaka.Masuha
ReplyDeleteAsante sana Mkuu
ReplyDelete