MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Thursday, 27 July 2017

viongozi wahakikishe wananchi wanajiunga na Bima ya Afya.



Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Halima Dendego akimpa maelezo ya umuhimu wa kadi ya Bima ya Afya mmoja wa wateja wapya wa huduma hiyo kabla ya kumkabidhi wakati wa  ziara yake ya kikazi wilayani Newala

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego ameagiza viongozi wa ngazi zote katika Halmashauri kuhakikisha wanasimamia wananchi kujiunga na Bima ya Afya ya Jamii CHF. Amesema hiyo ndiyo njia bora ya kuwezedha jamii kuwa na afya bora.

Dendego ameyasema hayo leo wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Kitangari wilayani Newala. Amesema ili kuhakikisha utekelezaji wa suala hilo unakuwa wa haraka na ufanisi zaidi, kila kiongozi katika ngazi ya kijiji ahakikishe amejiunga na Bima ya afya ili kujenga matumaini kwa anaowahamasisha. Amesema kiongozi  asiye kuwa na kadi hiyo hafai kuwa kiongozi kwani haiwezekani kiongozi kuimba wimbo ambao yeye mwenyewe hauwezi. 

‘Ndugu wananchi, serikali iko tayari kuwahudumia watu. Ndio maana imeweka utaratibu wa kuchangia shilingi 10,000 kwa ajili ya kupata Bima ya Afya ambayo inamuwezesha mwanajamii yeye pamoja na familia yake ya watoto wanne kupata matibabu bure.
Aidha, Dendego amewataka Waganga Wakuu wa Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati kuhakikisha dawa zinakuwepo muda mrefu. Amesema ni marufuku mgonjwa mwenye kadi ya CHF kukosa dawa kwani serikali imeweka miundombinu bora kuhakikisha dwa zinakuwepo muda wote.

Mkuu wa Wilaya ya Newala Mhe. Aziza Mangosongo akizungumza na wananchi

Awali akizungumzia agizo hilo Mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Aziza Mangosongo amesema wamejipanga na kwamba agizo la Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa watalitekeleza kwa haraka . 

Kwa upande wake mkazi wa kijiji cha Mnyambe Somoe Hassan amesema moja ya changamoto inayowafanya wasijiunge ilikuwa ni kutokuwa na imani na huduma zinazotolewa katika hospitali kwani mara nyingi wamekuwa wakiambiwa hakuna dawa. ‘Kwa kauli hii aliyoitowa Mkuu wa Mkoa sasa tuna matumaini mapya’. Amesema Somoe.
Mheshimiwa Halima Denego yuko katika siku ya pili ya ziara ya kikazi siku Nne wilayani Newala.

 RC Mtwara akikabidhi vitanda 20 na magodoro 20 yaliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa ajili ya Wilaya ya Newala

No comments:

Post a Comment