MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Friday, 4 August 2017

RC Mtwara atoa saa 48 watuhumiwa wa kuuza salfa feki kujisalimisha






Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Halima Dendego ametoa saa 48 kwa wote wanaohusika na tuhuma za kusafirishaji wa Pembejeo zilizoisha muda wake kutoka ghala la Naliendele kwenda wakulima wilayani Tandahimba warejee kujibu tuhuma zinazowakabili.

Amesema pamoja na kwamba suala hilo ameshalikabidhi kwa kamanda wa polisi mkoa bado anaagiza wote wanaohusika na tuhuma hizo hata kama wako nje ya mkoa warejee ndani ya saa 48.
Agizo hilo amelitoa leo baada ya uchunguzi uliofanywa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa katika ghala linalotuhumiwa kusafirisha Salfa hiyo kujiridhisha na utata wa ubora wa pembejeo hiyo.
Salfa hiyo inayokisiwa kufikia tani 20 ilisafirishwa kutoka ghala hilo lililoko eneo la Naliendele mkoani Mtwara kuelekea Wialayani Tandahimba na kukamatwa Juni 30 mwaka huu.
Mheshimiwa Dendego amesema ameshatoa maelekezo kwa wakulima wasitumie dawa hiyo na kwamba wataendelea kusimamia kuhakikisha mkulima anapata bidhaa yenye ubora stahili.
Aidha Mheshimiwa Dendego ameeleza kuwa ataundwa kikosi kazi kufanya uchunguzi iwapo salfa iliyoenda kwa wakulima ni tani 20 pekee.
Uamuzi huo unafuatia taarifa za wasimamizi wa ghala hiyo kwamba walisafirisha tani 20 pekee kati ya tani 75 zilizokuwemo. 

Akizungumzia kuhusu tuhuma hizo Mhandisi wa Kilimo Mkoa Aman Lusake amesema Salfa hiyo ilikamatwa mwishoni mwa mwezi wa 6 mwaka huu ikiwa imesafirishwa kwenda Tandahimba na kwamba baada ya taarifa hizo kufikishwa kwa mamlka ya uchunguzi wa ubora wa salfa hiyo TPRI wataalamu hao walitoa taarifa kuwa salfa hiyo imeisha muda wake na kwamba haistahili kwa matumizi. 

Kwa upande wake Mkaguzi wa Ndani Bodi ya Korosho Mary Mapunda amesema yeye aliambiwa kuruhusu salfa hiyo kwenda kwa wakulima pasipo kujua iwapo ina ubora stahili. Aidha hata mnunuzi aliyekuja kuichukua alielekezea kuihitaji kwa ajili ya matumizi ya bustani.

Video ya tukio zima hii hapa chini.


No comments:

Post a Comment