MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Tuesday 25 February 2020

DC Tandahimba apiga marufuku michango ya shule isiyofuata utaratibu


Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Mhe. Sebastian Waryuba amepiga marufuku michango inayokwenda kinyume na maagizo yaliyoko katika miongozo ya elimu shuleni.  Agizo hilo amelitoa jana Februali 24, 2020 kufuatia malalamiko ya wananchi wakati wa ziara yake ya siku moja kusikiliza kero za wananchi na kukagua maendeleo ya shule. Wananchi hao walidai kuwa baadhi ya shule hasa za sekondari walimu wamekuwa wakiomba michango ambayo inaleta usumbufu kwa wazazi.

Mhe. Sebastian Walyuba akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mmeda
Mheshimiwa Walyuba amesema michango inayokwenda kinyume na utaratibu inaweza kuwa chanzo cha wanafunzi kushindwa kuhudhuria shuleni na kwamba inapingana na dhana ya elimu bila malipo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya Tano kupitia kwa Rais, Dkt.  John Pombe Magufuli.

Katika ziara hiyo ya siku moja Mhe. Walyuba alitembelea vijiji vya Mmeda, Mabeti na Mkola akiwa amembatana na maafisa wa halmashauri, wataalam wa TANESCO na TARULA. Aidha, alihimiza Amani, kufanya kazi kwa bidi na kuwataka wazazi ambao Watoto hao hawajaripoti shuleni wakamatwe na kufikishwa mahakamani.
 Mhe. Waryuba akihamasisha wanafunzi kuwa raia wema kupitia mafunzo ya darasani shule ya Msingi Mmeda 
wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Sebastian Walyuba. (hayupo pichani)

No comments:

Post a Comment