Awali akikabidhi pikipiki hizo
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa amewataka Maafisa Tarafa
kufanya kazi kwa kujituma na kwamba serikali inawatahamini. Aidha amewataka wahakikise
wanazitunza kwa kuzifanyaia matengenezo ya mara kwa mara ili zidumu na kutimiza
malengo yaliyokusudiwa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti,
Maafisa Tarafa, Octaviani Lyapembile wa Tarafa ya Mikindani pamoja na Marko
Mapunda wa Tarafa ya Mangaka Nanyumbu wamesema wamepokea msaada huo kwa furaha
na kwamba serikali itegemee mabadiliko chanya ya utendaji kazi. Wanasema
walikuwa na changamoto kubwa ya usafiri kutokana na ukubwa wa maeneo yao ya
utawala jambo ambalo lilikuwa likiwalazimu kutembea kwa miguu.
No comments:
Post a Comment