Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa mara baada ya kuuwasili Uwanja wa ndege wa Mtwara
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa
Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) amezindua mradi wa umeme ambao utaunganisha mikoa
ya Mtwara na Lindi katika Gridi ya Taifa. Kabla ya mradi huu Mikoa hii miwili ilikuwa
ikipokea nishati hiyo kutoka kwenye kituo cha kuzalisha umeme kilichoko Mtwara
mjini ambapo mahitaji ya Mikoa ya Lindi na Mtwara kwa sasa yamekuwa yakitajwa
kuwa ni megawati 16.5.
Akizindua mradi huo katika kituo cha kuunganisha nishati hiyo
kijijini Mahumbika Lindi Mheshimiwa Waziri Mkuu amesema kwamba mradi huo ni
miongoni mwa ahadi ya serikali ya awamu ya tano ya kuhakikiisha inatatua
changamoto zote zinazokwamisha maendeleo.
Amesema hiyo ni fursa muhimu kwa mikoa ya Lindi na Mtwara
kualika wawekezaji hasa baada ya kuondokana na tatizo la nishati ya umeme.
Baada ya zoezi hilo lililofanyika huko Lindi Mheshimiwa
Waziri Mkuu aliyekuwa na ziara ya siku moja katika mikoa hii miwili amezindua
upanuzi wa kituo cha kufua umeme kilichoko Mtwara mjini ambapo serikali ya
awamu ya tano imeongeza mashine mbili zenye uwezo wa kufua megawati 2 kila
moja. Hilo linakifanya kituo hicho kilichokuwa na uwezo wa kuzalisha megawati
18 kuanza kuzalisha megawati 22.
Kwa miezi ya hivi karibuni mikoa ya Mtwara na Lindi ilikumbwa
na changamoto kubwa ya kukatika katika kwa umeme hasa kutokana na kuharibika
kwa baadhi ya mashine katika kituo hicho. Kufuatia hali hiyo serikali iliahidi
kununua mashine mbili na kuzifanyia matengenezo mashine zilizoharibika. Ahadi
hiyo imekamilika.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majailiwa Majaliwa akishangilia pamoja na wanamtwara mara baada ya uzinduzi wa usafirishaji wa mafuta kupitia Bandari ya Mtwara
Baada ya zoezi la miundombinu ya Umeme Mheshimiwa Waziri Mkuu amezindua usafirishaji wa mafuta kupitia
Bandari ya Mtwara. Kabla ya hatua hii mkoa wa Mtwara na mikoa yote ya kusini
ilikuwa ikipata mafuta kutokea Bandari ya Dar es Salaam hali ambayo ilikuwa
ikiifanya nishati hiyo kuuzwa kwa bei ya juu kutokana na gharama za
usafirishaji kutoka Dar es Salaam.
Akizungumzaia mafanikio ya hatua hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara
Mheshimiwa Gelasius Byakanwa amesema mambo yote haya mawili yanatoa fursa ya
mkoa kuchagamuka zaidi. Mafuta haya yanatarajiwa kuchukuliwa hapa mkoani na
kusafirishawa ndani na nje ya nchi. Ametoa wito kwa wawekezaji kuja mkoani
Mtwara kwani Fursa kubwa zimefunguka.
No comments:
Post a Comment