MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Monday 19 March 2018

RC Mtwara atishia kuwanyima nyumba walim wasiojali

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa ameagiza walimu wote mkoani Mtwara waliopewa nyumba za kuishi kuingia mikataba na Halmashauri kwa ajili ya utunzaji wa nyumba hizo. Agizo hilo amelitoa jana wakati akikagua nyumba za walimu wa shule ya msingi Lulindi 1 iliyoko kijiji cha Muungano kata ya Lulindi Wilayani Masasi mara baada ya uzinduzi wa zoezi la upandaji miti kimkoa lililofanyika kijijini hapo.
Mhe. Byakanwa akionesha moja ya nyumba ya Mwalim katika shule ya Msingi LulindiMoja ambayo nyavyu za madirisha zimeharibika bila kufanyiwa matengenezo

Mheshimiwa Byakanwa amesema hatavumilia mwalimu anayepewa nyumba bure kushindwa kuitunza. Anasema ni bora nyumba hiyo akapewa mwalimu mwingine mwenye moyo wa kuitunza kuliko Mwalimu anayesubiri serikali imfanyie kila kitu.
 
Amesisitiza kuwa serikali imeonesha kujali ndiyo maana imewajengea nyumba na kuwapa waishi bure hivyo haipendezi mwalimu anayeishi katika nyumba hiyo kuendelea kusubiri serikali irekebishe mambo madogomadogo ikiwemo nyavu za madirisha zilizochoka.

Licha ya agizo hilo Mheshimiwa Byakanwa ameahidi kuchangia bati za vyumba vitatu vya madarasa kwa sharti la kuwataka wanakijiji kuhakikisha wanajenga boma. Pia ameitaka serikali ya kijiji hicho kuandaa tofari za kutosha nyumba mbili za walimu ambapo amemutaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Juma Satma kuchangia ujenzi wa nyumba hizo.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Juma Satma  amesema agizo hilo wamelipokea na kwamba wako tayari kulifanyia utekelezaji.
Awali akiwasilisha kero ya shule hiyo Rajab Abdelimali Soni, mkazi wa kijiji hicho alimuomba Mkuu wa Mkoa kutembelea shule hiyo kutokana na changamoto ya miundombinu ya shule hiyo.
Amesema shule hiyo ni kongwe lakini bado inatatizo la miundombinu ya nyumba za walimu pamoja na vyumba vya madarasa jambo ambalo limekuwa likisababisjha walimu kuishi mbali na mazingira ya shule na hivyo kuathili utendaji kazi.


No comments:

Post a Comment