MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Tuesday 20 February 2018

Wamakonde na Tamaduni za kuzika wafu wao Wima


Anaandika Karl Weule kwenye kitabu chake ‘Native Life in East Africa.’ Tafsiri ya Kiingereza kutoka kijerumani imetolewa na Alice Werner. Kimechapishwa mwaka 1909 na New York D’ Appleton and Company. Tafsiri ya Kiswahili isiyo rasmi inatolewa na Evaristy Masuha. 

Karl Weule
Anaanza Weule kwa kusimulia. 

Niliingia Newala Mwishoni mwa Septemba 1906. Kubwa lililonishangaza ni hali ya maisha ya wakazi wa Mji huu ambao wanaishi katika mazingira ya shida kubwa ya maji. Mimi na mwenzangu Knudsen tulijiuliza maswali kwa nini watu hawa wamekuwa na ujasili wa kuishi katika misitu mikubwa yenye shida ya maji kiasi hiki. 

Hata hivyo nilipata picha halisi ya simulizi niliyokuwa nayo tangu nikiwa ujerumani juu ya mapori makubwa yenye wanyama hatari ambayo yamewazunguka watu wa Ujerumani ya Afrika Mashariki. (German East Africa).

Wakati tunaingia mji huu tumetembea umbali mrefu tukipita mapori makubwa. Ishara ya uwepo wa watu katika eneo tulilokuwa tukilikaribia ni sauti za shoka na mapanga yakiangusha misitu mikubwa. Kazi hii ilikuwa inafanywa na wanafamilia wote ikiwemo baba, mama, watoto, na wakwe.

Huu ndio utaratibu wa kilimo cha watu hawa, kufyeka kisha kuchoma moto. Baada ya kuteketeza msitu, wenyeji hawa hupanda mazao tayari kwa kupalilia hadi kuvuna.


Wamakonde na tamaduni ya kuzika wafu wao wima.
Baada ya kuwapata wenyeji katika eneo hili ambalo tulitambulishwa kuwa linaitwa Mahuta, utafiti wangu ulianzia kutaka kujua kwa nini wanakuwa na ujasiri wa kuishi katika maeneo haya yenye hatari ya wanyama na shida kubwa ya maji.

Mwenyeji wangu alinieleza kuwa ipo historia ndefu ambayo inawafanya wasiishi katika maeneo ya maji. Alieleza kuwa simulizi walizozipata toka kwa babu zao ni kwamba kabla ya kuwa kijiji eneo hilo lilikuwa pori lenye msitu mkubwa na wanyama wakali. Mwanzo wa maisha katika mji huo ulianza baada ya ujio wa mtu mmoja aliyetokea kusikojulikana. Mtu huyo alikuwa na nywele nyingi ambazo zilikuwa hazichanwi. Pia alikuwa akioga mara chache na kula kidogo sana.

Baada ya kuanzisha makazi yake pale Mahuta mtu huyo alichonga kinyago cha mwanamke ambacho alikisimamisha katikati ya mji wake. ilipokuwa inafika usiku, kinyago au sanamu hiyo ilikuwa ikibadilika kuwa mwanamke ambaye walikuwa wakitelemka naye mto Ruvuma kwa ajili ya kuoga na kuchota maji.
Baada ya muda mwanamke huyo alizaa mtoto wa kiume kisha wawili hao wakaamua kuhamisha makazi yao. Wageni hao walitembea hadi wakavuka mto Mbemkuru ambapo yule mama alizaa mtoto wa pili akiwa amefariki. 

Hali hiyo iliwasikitisha wageni hao wakalazimika kurudi Mahuta ambapo walizaa tena mtoto wa tatu. Mtoto huyu alikuwa na kuishi akiwa na afya njema. Baada ya muda familia hiyo ilipanuka na kutengeneza ukoo ambao waliuita ‘Wamatanda’. Wamatanda hawa walipokuja kuongezeka ukatokea ukoo ambao nao ulipanuka na kujiita wamakonde.

Mwenyeji wangu aliendelea kuwa huyo Babu asiyenyoa nywele alipofikia siku za mwisho wa maisha yake, alitoa agizo kwa watoto wake kuhakikisha wanawazika ndugu zao kwa kuwasimamisha wima kaburini ikiwa ni kukumbuka ya asili ya bibi yao (sanamu iliyokuwa ikipata uhai usiku). Pia akawapa onyo wasikae karibu na mto au kwenye chanzo chochote cha maji.

 Aliwaeleza kuwa mauti ya binadamu yamejaa na yanaishi kwenye chanzo cha maji hivyo wasithubutu kuishi maeneo kama hayo. Hali hiyo ndiyo iliwafanya waendelee kuishi hapo Mahuta.


Tafadhali Toa comment yako hapo chini

4 comments:

  1. Kweli tumetoka mbali katika tamaduni zetu

    ReplyDelete
    Replies
    1. This comment has been removed by the author.

      Delete
  2. OK, NIMEPATA FAIDA KUJUA HISTORIA


    ASANTE

    ReplyDelete
  3. Je historia ya vinyago vya komakomde imetokea wapi, nashukuru sana

    ReplyDelete