Kanisa
la Kiinjili la Kilutheli Tanzania Dayosisi ya Kusini Mashariki Usharika wa
Kanisa Kuu wamemtunuku Tuzo ya Mwanamke Jasiri Mkuu wa MKOA wa Mtwara. Mhe.
Halima Dendego ikiwa ni kutambua mchango wake Mkubwa ktk kusukuma maendeleo ya
Mtwara.
Tuzo
hiyo iliyotolewa Jana katika kanisa la KKKT lililoko Mjini Mtwara lilishuhudiwa
na viongozi mbalimbali wa mkoa pamoja na waimbaji kutoka makanisha mbalimbali
ikiwemo kwaya ya Kanisa Katoliki Parokia ya Mtwara.
Akizungumza
wakati wa kumkabidhi tuzo hiyo, Askofu Mkuu wa Dayosisi hiyo, Lucas Mbedule
Juda amesema vipo vielelezo vya mambo mengi makubwa aliyoyafanya Mhe.
Dendego ambayo ni kielelezo cha ujasiri wake katika kusimamia haki.
Amesema
yeye mwenyewe Askofu amekuwa mfuatiliaji wa karibu wa kazi za Mheshimiwa Mkuu
wa Mkoa tangu akiwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga kabla ya kuhamishiwa hapa Mtwara
miaka mitatu iliyopita.
Akinukuu
maandiko matatatifu kutoka kwenye kitabu cha “Marko 16.1-4 Mbedule amesema kitabu
hicho kinaonesha ujasiri mkubwa unaohitajika katika kuitafuta haki jambo ambalo
Mheshimiwa Dendego ameliweza.
“Hata
sabato ilipokwisha kupita, mariamu Magdalena na Mariamu mamaye Yakobo, na
Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka. Hata alfajili mapema siku ya
kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza. Wakasemezana wao
kwa wao, ni nani atakayetuviringishia lile jiwe mlangoni pa kaburi? Hata
walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuviringishwa, nalo lilikuwa
kubwa mno.”
Anasema
andiko hilo linawataja baadhi ya watu ambao ni maarufu kwa kukatisha tamaa wenzao
katika jitihada za mapambano ya ukombozi kama ambavyo mmoja wa wanawake hao alivyojaribu
kuwakatisha tamaa wanawake wenzake lakini ujasili wa wale akina mama
haukukatishwa tamaa katika kuliendea jiwe lililofunika mwili wa Yesu.
Akizungumzia
hati aliyoitoa Askofu Mbedule amesema hati hiyo inatambulika kama HATI YA
ASKOFU YA HESHIMA YA JUU ambayo hutolewa Mara chache, kwa watu wachache hasa
baada kujiridhisha na utendaji uliotukuka kwa mhusika.
Kwa
upande wake Mhe. Dendego ambaye amekuwa Mkuu wa MKOA huu kwa miaka mitatu sasa
anasema tuzo hiyo imempa nguvu ya kuendeleza jitihada zake kutetea maslahi ya
wengi hasa wanyonge. Amesema wapo watu wengi ambao wamekuwa wakimkatisha tamaa
katika jitihada zake. Wengine wamekuwa wakimbeza na hata kumsingizia vitu vingi
lakini kwa heshima aliyopewa na kanisa hilo imempa nguvu na anajiona ni mpya
katika mapambano.
Mheshimiwa
Dendego amewataka akina mama wengine wajipe moyo wa mapambano kwani katika
kufikia ushindi lazima mtu ajitowe mhanga.
Kwa
upande wao wananchi waliokuja kushuhudia tukio hilo wamepongeza uamuzi wa
kanisa hilo kwamba umefanyika katika muda muafaka na kwa usahihi kabisa.
Mwalimu
Frank Komba wa shule ya Msingi magomeni Mkoani Mtwara anasema amekuwa
akifuatilia kwa karibu kazi za Mkuu wa Mkoa tangu amekuwepo hapa na
amefurahishwa na mambo mengi likiwemo suala la kusimamia elimu huku akiwabana
wananfunzi wanaopata ujauzito na wanaowapa. Anamshauri Mkuu huyo aendelee na
jitihada hizo kwani nidhamu kwa wanafunzi imejengeka sasa.
Joseph
Haule Mkazi wa Mangamba Mtwara mjini anaongeza kuwa Mkuu wa Mkoa ameweza kuzuia
suala la kuwatumikisha watoto wa kike katika mtindo wa wafanyakazi wa ndani na
hata wakati mwingine kuwageuza chombo cha starehe. Amemtaka Mheshimiwa Magufuli
aendelee kumuunga mkono na asimuhamishe mkoani Mtwara.
Aidha
Viktoria Daudi mkazi wa Mtwara anaguswa na kazi za Mkuu wa Mkoa katika suala la
usimamizi mzuri wa zao la Korosho. Anasema kabla yake kulikuwa na ukiukwaji wa
taratibu za ununuzi na uuzaji wa korosho ambapo wanunuzi wengi walikuwa wakinunua
korosho katika mfumo usio rasmi na hivyo kuwanyima mapato stahili wakulima. Baada
ya usimamazi wa Mheshimiwa Dendego suala hilo limepungua kwa kiasi kikubwa na
sasa wananchi wanafurahia mfumo wa stakabadhi ghalani.
Video hiyo hapo chini.
No comments:
Post a Comment