MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Saturday 26 November 2016

Kaimu Katibu Tawala Mkoa aongoza Usafi wa Mazingira Nanyumbu.


Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara, Renatus Mongogwela amewaongoza mamia ya wananchi wa Wilaya ya Nanyumbu katika shughuli ya Usafi kimkoa uliofanyika katika Mji wa Mangaka wilayani Nanyumbu. zoezi hili limefanyika ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali la usafi kila jumamosi ya mwisho wa mwezi.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mtwara, Renatusi Mongogwela (wa tatu kushoto, shati jeupe) akiwaongoza wananchi kuelekea uwanja wa CCM nanyumbu ili kupata nasaha za mwisho baada ya zoezi la usafi.

katika zoezi hilo lililohudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Jimbo la nanyumbu Dua William Nkurua, Mongogwela amesisitiza  zoezi la Usafi kuwa endelevu kwa ngazi zote. Amesema haipendezi kusubiri viongozi kuwaamusha wanananyumbu kufanya usafi Wakati wote wamesoma na wanatambua kuwa usafi ni afya. 

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara, Renatus Mongogwela akihutubia wananchi mara baada ya usafi.

Sambaba na usafi huo Mongogwela amewaongoza wana Nanyumbu  kupanda miti katika chanzo cha maji yanayohudumia vijiji vya Mara, Sengenya na Ngalinje.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara Renatus Mongogwela akipanda Mti katika chanzo cha maji cha Mara, Sengenya na Ngalinje.

Mbunge wa jimbo la Nanyumbu Dua William Nkurua akipanda Mti.


Mhandisi wa mazingira mkoa, Falaura Kikusa akipanda Mti.


Mbunge wa jimbo la Nanyumbu Dua William Nkurua (wa kwanza kushoto)akiwasalimia wananchi mara abaada ya zoezi la usafi.

Diwani wa kata ya Sengenya (mwenye gauni jekundu) akiwasalimia wananchi mara baada ya usafi wa mazingira.


Bwawa la maji la Mara Sengenya.




2 comments:

  1. inawezekana pakafugwa samaki katika hilo bwawa na kupunguza uwezekano wa kukumbwa na balaa la ukosefu wa chakula ?

    ReplyDelete
  2. Wataalamu wa Uvuvi wanaweza kuangalia japo lengo lake halikuwa kwa ajili ya samani bali huduma ya maji kwa wakazi

    ReplyDelete