Serikali ya Mkoa wa Mtwara imeanzisha operation maalumu ya kuwakamata wafanyabiashara wanaouza sukari kinyume na maelekezo ya serikali. Zoezi hilo lililoanza jana limeweza kuwakamata wafanyabiashara wanane ambao walikutwa wanauza sukari kwa bei ya hadi shilingi 3600 kwa kilo moja.
Akizungumza mara baada ya kumuapisha Mhe. Dunstan Kyobya aliyeteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe Gelasius Byakanwa amesema operation hiyo ni endelevu kwa mkoa mzima. Amewataka wananchi watowe taarifa kwa jeshi la polisi juu ya wafanyabishara wanaokiuka maagizo.
maelezo zaidi fungua hiyo video au tembelea youtube channel ya Mtwara RS. Usisahau kusubscribe huko.
No comments:
Post a Comment