Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa
Gelasius Byakanwa ametoa wito kwa Taasisi, Mashirika na watu binafsi
wenye uwezo wa kutengeneza barakoa (Mask) watengeneze kwa wingi. Wito
huo ameutoa leo Aprili 17, 2020 wakati akipokea msaada wa vifaa vya
kujikinga na maradhi ya COVID-19 kutoka kwa kampuni ya Beijing
Construction and Engineering Group CO. LTD inayoshughulika na upanuzi wa
uwanja wa Ndege wa Mtwara.
Amesema mahitaji ya vifaa hivyo kwa sasa
ni makubwa hasa kwa watoa huduma na watu wote ambao kila siku wanafanya
kazi ya kukutana na watu. Aidha, amesisisitiza jamii kuendelea
kujikinga na ugonjwa huo kwa kuzingatia tahadhari zote ikiwemo kuvaa
barakoa huku akiwasisitiza wageni wanaotembelea ofisini kwake
kuhakikisha wanavaa barakoa.
“..na mimi kama Mkuu wa Mkoa,
tutakapoanza wiki inayofuata, hakuna mtu atakayefika kwenye ofisi yangu
bila kuvaa Mask. kuanzia jumatatu tarehe 20, kila mtu atakayefika kwenye
ofisi ya Mkuu wa Mkoa atapaswa kuwa amevaa Mask.” Amesema Byakanwa.
Naye Meneja wa kampuni ya Beijing
Construction Cui Rui Tao ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa hatua
inazochukua dhidi ya ugonjwa wa COVID-19. Amesema wameona umuhimu wa
kusaidia jitihada hizo kwa kutoa msaada wa Barakoa elfu moja, galoni 10
za lita tanotano Pamoja na vitakasa mikono.
Kutazama video ya makabidhiano. Bonyeza hapo. https://www.youtube.com/watch?v=CQXKWDd3r7E
No comments:
Post a Comment