Umaarufu wa mkoa wa Mtwara katika kula nyama ya panya ni fursa mojawapo ya kuvutia utalii mkoani hapa. Hilo litawezekana iwapo jamii ya watu wanaotumia chakula hicho watawekewa mazingira mazuri ya kujitangaza na kukitangaza chakula hicho kupitia matukio mbalimbali ikiwemo ‘Panya festival’ au panya Choma.
Akizungumza katika kipindi cha
safiri nasi kilichokuwa kikirushwa moja kwa moja kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mtwara leo, Mhe. Gelasius Byakanwa amesema hilo ni mojawapo ya malengo yake
kuhakikisha fursa mbalimbali za mkoa wa Mtwara ikiwemo ulaji wa nyama ya panya
unatumika kama kivutio. Aidha katika ratiba yake amepanga kabla ya mwezi wa
saba mwaka huu kuandaa tukio ambalo na yeye atashiriki kula nyama hiyo.
Anasema fursa hiyo inaweza
kuwavuta watu wengi kutoka ndani na nje ya nchi na kuufanya mkoa wa Mtwara
kujulikana zaidi. Aidha itatoa fursa ya kufanya maboresho katika chakula hicho
katika mtindo bora na wa kisasa zaidi.
“Kwa nini tusitangaze, isiwe rasmi kwamba panya ni chakula,
tukawakaribisha mikoa mingine kwamba njooni Mtwara tule panya. Lakini kama sisi
wenyewe tukikitambua na kukihalalisha kuwa hiki ni chakula bila kuitenga ile
jamii… so long as hakina madhara kwa afya ya mtu, na pengine imani yako haizuii,
mimi sioni sababu kwa nini tusikichukuwe na chenyewe kikawa kivutio”.
Amesema Mhe.Byakanwa.
Mhe. Byakanwa ambaye ni Mwenyeji
wa Mkoa wa Kagera ametolea mfano mkoa huo kwamba ni maarufu kwa ulaji wa Senene
na kwamba chakula hicho sasa kimevuka mipaka kutoka Bukoba hadi nje ya nchi.
“Kule Bukoba tunakula senene, mwanzoni senene walionekana wanaliwa
Bukoba tu lakini sasa kila sehemu wanakula, mpaka wengine wanakuwa exported nje
ya nchi. Kwa nini panya nao wasiwe hivyo?
Nyama ya panya ni chakula maarufu
mkoani Mtwara huku wilaya ya Masasi ikitajwa kuongoza katika ulaji wa nyama
hiyo.
No comments:
Post a Comment