Wiki hii Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa
amefanya ziara katika Halmahauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kukagua miradi
mbalimbali ya maendeleo pamoja na kusikiliza kero zinazohusiana na masuala ya
ardhi. Ziara hiyo ya siku mbili ilianza tarehe 27 na kukamilika tarehe 28.
Moja ya mgogoro aliousikiliza ni kuhusu mpaka kati ya makazi
ya wananchi na eneo la uwanja wa ndege.
Baada ya kusikiliza pande zote Mheshimiwa Byakanwa ameunda
Kamati Maalumu ambayo ameiagiza kupitia nyaraka zote za migogoro hiyo na
kumshauri nini kifanyike.
Hapa ni baadhi ya matukio yaliyojitokeza katika ziara hiyo;
Mheshimiwa
Byakanwa akipokea nyaraka za utetezi toka kwa Meneja wa Uwanja wa Ndege Emily Simbachawene
2. Mheshimiwa
Byakanwa akikagua ujenzi wa ofisi ya Mtendaji wa Kata Jangwani. Halmashauri ya
Manispaa ya Mtwara mikindani imeweza kujenga ofisi za watendaji kwa kata zote
18 zinazounda Halmashauri hiyo.
Ujenzi huu unakusudia
kuondoa changamoto ya mlundikanao wa magari katika kituo cha sasa kilichoko
Mtwara mjini ambacho kinapokea magari yanayoenda mikoani/Wialayani na daladala.
Mheshimiwa
Byakanwa akipokea maelezo ya ujenzi wa ukuta wa ofisi Mkurugenzi wa Manispaa.
Ujenzi huu unakusudia
kuimarisha usalama wa ofisi na kupunguza muingiliano wa watumishi na watu wa nje.
Ujenzi
wa zahanati Mbawala chini.
Wananchi wametoa ardhi ekali 5, kusaidia nguvu kazi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo.
Mheshimiwa Byakanwa akiwazawadia fedha taslimu wanafunzi wa shule ya Msingi Singino waliojibu kwa ufasaha maswali ya chemsha bongo aliyowauliza wakati wa ziara hiyo
Wananchi wametoa ardhi ekali 5, kusaidia nguvu kazi kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo.
Mheshimiwa Byakanwa akiwazawadia fedha taslimu wanafunzi wa shule ya Msingi Singino waliojibu kwa ufasaha maswali ya chemsha bongo aliyowauliza wakati wa ziara hiyo
Mwenyekiti wa Mtaa wa Mbawala Chini (katikati) pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa (Kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhehimiwa Evod Mmanda mara baada ya ukaguzi wa ujenzi wa Zahanati.
No comments:
Post a Comment