Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Gelasius Byakanwa ametoa Msaada wa chakula cha Krismas kwa wananchi wenye Mahitaji maalumu mkoani Hapa.
Akikabidhi chakula hicho kwa Jumuia ya SANT
EGIDIO iliyoandaa tukio la chakula hicho, Mhasibu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mtwara Norbert Shee ambaye alikuwa akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa amesema
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameguswa na tukio hilo, hivyo ameamua kutoa mafuta ya
Kula, Maharage, Mchele na nyama vyote vikiwa na thamani ya shilingi laki tano.
Amesema wenye kuhitaji msaada ni wengi hivyo
kunahitajika jitihada za pamoja kwa wadau mbalimbali ili kuwafikia wana jamii
wote na kwamba Mkuu wa Mkoa alitamani kujumuika pamoja nao lakini kutokana na
kuwa nje ya Mkoa kikazi hakuweza kufanya hivyo.
‘Naamini roho ya upendo ndiyo iliyowasukuma
Jumuia ya Sant Egidio kuandaa tukio hili. Ni vema jamii zingine nazo zikaiga
jambo hili kwani ni jema na linapendeza mbele za Mungu’.
Akipokea msaada huo uliotolewa katika ukumbi wa
Kanisa katoliki Mtwara, Mratibu wa Sant Egidio Mkoani Mtwara, Felician Ponsian
kwa niaba ya Taasisi nzima ametoa shuklani kwa msaada huo na kwamba ni ishara
kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Mkoa mwenyewe wako pamoja na wenye
mahitaji maalumu. amesema taasisi hiyo imekuwa ikifanya hivyo kutokana na
kutambua uwepo wa mahitaji makubwa ya jamii na hivyo wao wameamua kuchukua
jukumu hilo kuwaleta pamoja katika furaha.
Kwa upande wake Naomi saidi Mkazi wa Miembeni
Mjini Mtwara ambaye ni mmoja wa washiriki wa chakula hicho amesema anashukuru
wanapoona viongozi wao wakiwa karibu nao. Amewata waendelee na moyo huohuo.
No comments:
Post a Comment