MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Thursday 31 August 2017

Maazimisho ya miaka 53 ya JWTZ Agost 31, 1017 Mashujaa Mtwara

Majeshi yote nchini yametakiwa kuwa na umoja, ushirikiano na mshikamano ili kutimiza majukumu yao. Hayo yamesemwa leo na Brigedia Jenerali George Msongole wa Brigedi ya Kusini wakati wa maazimisho ya miaka 53 tangu kuanzishwa kwa jenshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) yaliyofanyika uwanja wa Mashujaa mjini Mtwara. 

Amesema lengo la kuanzishwa kwa majeshi yote ni kutoa huduma kwa wananchi wa Tanzania hivyo mshikamano ni jambo la muhimu.

Akizungumzia Jeshi la Wananchi wa Tanzania amesema Jeshi hilo kama linavyojulikana ni jeshi ambalo limetokana na watanzania wenyewe hivyo linapaswa kuenzi malengo ya waasisi ambayo ni pamoja na uzalendo. 


Katika maazimisho hayo yaliyojumuisha majeshi mbalimbali ya hapa nchini Msongole amesema historia ya jeshi la Wananchi wa Tanzania ilianzia tangu likiitwa King African Rifle ambalo lilianzishwa na Mkoloni kwa lengo la kulinda maslahi ya mkoloni kisha kubadilishwa kuwa Tanganyika Rifle na hatimaye Jeshi la Wananchi wa Tanzania lililoanzishwa Septemba 1, 1964.


 Msongole amesema majeshi yote yanapaswa kutambua kuwa malengo yao ni ustawi wa taifa na hivyo kuacha tofauti zao na kuwa kitu kimoja.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mheshimiwa Halima Dendego amelishukuru Jenshi la Wananchi wa Tanzania na majeshi yote kwa ushirikiano wao katika kufanikisha shughuli hiyo. Amesema yako mengi yaliyofanywa na Majeshi hapa Mtwara ambayo yanabaki kama kumbukumbu kwa taifa. Ametaja baadhi ya mambo hayo kuwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya usalama wa kituo cha kuzalisha Umeme eneo la Pwani ya Mnazi mara baada ya mafuliko ya bahari yaliyotishia usalma wake mwanzoni mwa mwaka 2015. 
Sherehe hizi zilitanguliwa na maandamano ya kilometa 10 ambapo raia waliungana na wanajeshi katika matembezi hayo kisha kuendesha zoezi la Upimaji wa Virusi vya Ukimwi na uchangiaji damu kwa hiari. 

Video ya Tukio zima Hii Hapa.


No comments:

Post a Comment