MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Saturday 24 December 2016

Korosho yote kuondoka Mtwara Januari 15.



Katika kuutafuta ukweli juu ya bandari ya Mtwara na hasa katika kipindi hiki ambacho kelele nyingi zimesikika zikipinga kuwa bandari hiyo ni ndogo kuweza kupokea na kusafirisha shehena ya korosho, Mwandishi wa Mtwarars.blogspot.com leo ameamua kufanya ziara ya kushtukiza katika bandari hiyo. 

Moja ya jambo la kufurahisha na kushangazani pale meli mbili kubwa zilivyokuwa zimepaki katika gati moja huku zote zikipakiwa na kushusha makasha tayari kwa kusafirishwa nje ya nchi. Muonekano wa meli hizi katika gati ya bandari hii zilipingana na simulizi nyingi za kupinga uwezo wa bandari hii.

Meli mbili kubwa zilizokuwa katika bandari ya Mtwara Wakati mwandishi wetu alipotembelea eneo hilo. (Muonekano wote uko katika clip ya video yenye mahojiano na viongozi wa bandari)


Akizungumzia uwezo wa bandari hiyo Kapteni Hussein Bakari Kasuguru ambaye pia ni Baharia kiongozi wa bandari za mikoa ya kusini amesema bandari ya Mtwara ina uwezo mkubwa kuhilimi mizigo yote inayosafirishwa kupitia bandari hiyo.

Amesema meli yoyote yenye urefu wa mita kuanzia 180 ina uwezo wa kutia nanga katika bandari ya Mtwara na kwamba bado eneo la ghati ya bandari ni kubwa kuweza kuhimili meli mbili kwa Wakati mmoja. Aidha bandari hiyo ina kina cha mita 9.5 ambayo pia ni sifa ya ziada ya kuifanya iwe moja ya bandari bora duniani.
Kapteni Kasuguru akizungumza na mwandishi wetu.


Kapteni Kasuguru ameeleza kuwa kutokana na sifa hiyo ndiyo maana amethubutu kuweka meli mbili ambazo zikiunganishwa kwa pamoja zina urefu wa futi 296.

‘Hiyo meli unayoiona ya Kota Nilam ina urefu wa futi 180 wakati meli hiyo ya  Al Dhakhira ina urefu wa mita 116. Ukijumlisha zote mbili unapata jumla ya mita 296. Kama bandari isingekuwa na uwezo huo hivi sasa tungekuwa tunalaumiana mitaani kwamba tumefanya lisilowezekana’. Amesisitiza kaptein Kasuguru.

Kapteni Kasuguru ambaye ana uzoefu wa miaka mingi katika kazi hii amesisitiza kuwa siku zote duniani mataifa yanakuwa na utaratibu wake katika kuendesha mambo.

‘Wakati wowote serikali ikiamua utaratibu lazima usingatiwe, ndiyo maana sina wasiwasi na serikali ya Tanzania kuamua kutumia bandari ya Mtwara ambayo mimi kama Kapteni mzoefu sikushangaa Wakati tamuko la kuitumia bandari ya Mtwara kusafirisha korosho zote zinazotoka mikoa ya kusini’. Linatolewa. Alisisitiza.
 Afisa utekelezaji mwandamizi Bandari ya Mtwara Robert Soko.



Kwa upande wake Afisa utekelezaji mwandamizi Bandari ya Mtwara, Robert Soko amesisitiza kuwa kasi ya usafirishaji wakorosho kwa musimu wa 2016/2017 imeongezeaka.
Ameeleza kuwa mwezi Desemba, 23 mwaka 2015 walikuwa wameshahudumia meli 10 wakati Desemba, 23 mwaka 2016 wameshahudumia meli 13.

Kwa upande wa shehena ya korosho, hadi Desemba, 23 mwaka 2015 walikuwa wameshasafirisha tani 67,000 wakati mwaka huu tayari wamefikia zaidi ya tani 80,000. Aidha meli mbili zilizopo zinataraji kusafirisha jumla ya tani 20,000 na kufanya usafirishaji kufikia zaidi ya tani 100,000.

Soko anasisitiza kuwa kwa kawaida musimu wa usafirihaji wa korosho kila mwaka huenda mpaka mwezi wa tatu lakini mwaka huu wamejipanga kuhakikisha hadi katikati ya mwezi Januari wawe wamesafirisha zaidi ya tani 150,000. Kwa kiasi hicho ni matarajio kuwa korosho yote inayotarajia kupitia bandari ya Mtwara itakuwa imesafirishwa nje ya nchi. 

Tazama video nzima hapa






No comments:

Post a Comment