MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Monday 6 April 2020

Sirro awahakikishia ulinzi wakazi Mtwara







Mkuu wa Jeshi la polisi nchini (IGP) Simon Sirro
amewahakikishia ulinzi na usalama wananchi wa mkoa wa Mtwara na kuwataka wafanye
kazi zao bila hofu yoyote. Ameyasema hayo leo Aprili 6, 2020 wakati wa ziara ya
viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini yenye lengo la kuangalia
namna walivyojipanga kukabiliana na uhalifu ndani ya nchi na mipakani.

“kitendo cha kuona wanakuja wanachinja watu
wetu lazima ifike mahali tuseme mwisho na iwe mwisho. Wao wametangaza ligi. Wametangaza
mapambano lazima na sisi tuwe tayari kwa mapambano”. Amesema Sirro.

Bonyeza hapo chini usikilize

No comments:

Post a Comment