MTWARA RS

FUATILIA TAARIFA MBALIMBALI ZINAZOHUSU MKOA WA MTWARA NA SEHEMU NYINGINE NDANI NA NJE YA TANZANIA, KWA MAWASILIANO E-mail: yustace.evaristy@mtwara.go.tz SIMU: +255 717 697 205

Wednesday 20 December 2017

Byakanwa aagiza Manispaa kutenga maeneo ya Viwanda


Sijawa Omary, Mtwara

MKUU wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa ametoa wiki tatu kwa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani hapa kuhakikisha wanatenga viwanja maalumu kwa ajili ya ujenzi wa viwanda hasa nchi inapoelekea katika uchumi wa viwanda.
 Mhe. Gelasius Byakanwa. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akizungumza na watumishi wa Manispa ya Mtwara Mikindani. (Hawapo pichani)

Mhe. Byakanwa ametoa agizo hilo wakati wa kikoa na madiwani pamoja na watumishi wa halmashauri hiyo kilichofanyika kwenye halmashauri hiyo.

Alisema kuwa, viwanja vyote vilivyopo kwenye halmashauri hiyo ambavyo vimetelekezwa na wamiliki kwa muda mrefu bila kufanyiwa mazingira ya usafi au huduma yeyote vichukuliwe kutokana na wamiliki wake kushindwa kumiliki rasilimali hiyo.

“Viwanja vingapi kama halmashauri mumetenga kwa ajili ya ujenzi wa viwanda? Nashangaa kuona tunaelekea katika uchumi wa viwanda na hakuna viwanja vya kutosha ambayo vimetengwa maalumu kwa ajili hiyo”, Alisema Byakanwa.

Panapotekea fursa hizo ni vema kufanya maandalizi mapema ili kuondokana na usumbufu unaoweza kujitokeza hapo  baadae katika rasilimali hiyo.

Sanjali na hilo mkuu huyo amezitaka halmashauri zote mkoani hapa kuhakikisha zinasimamia ipasavyo pesa zote za miradi ya maendeleo ili kufikia malengo yanayokusudiwa katika mkoa huo.

“Nataka kuona halmashauri zote zinasimamia vema miradi yote ya maendeleo kwenye halmashauri zetu kikubwa tuweze kufikia lengo tunalokusudia”,Alisema Byakanwa.

Kaimu Mkurugenzi katika halmashauri hiyo, Tamko Ally alisema yale yote yaliyoangizwa na Mkuu huyo kama halmashauri yatafanyiwa kazi kwa vitendo ili kufikia malengo husika.

Katika swala la kutenga na kuangalia viwanja ambavyo wamiliki wameshindwa kuvihudumia pia litafanyiwa kazi kwa umakini wake hasa nchi inapoelekea katika uchumi huo wa viwanda.

No comments:

Post a Comment